Friday, April 05, 2013

MAANDALIZI YA UZINDUZI WA KLABU YA MSASANI JOGGING TAREHE 7 APRILI, 2013 YAKAMILIKA

Zimebaki siku mbili tu kabla ya tukio kubwa la kimichezo, hasa linaohusisha mchezo wa mbio za pole pole kutokea ambapo klabu ya mchezo huo inayojulikana kama Msasani Jogging inatarajiwa kuwakutanisha zaidi ya wana-jogging 700 kutoka katika vilabu takriban 20 vya mkoa wa Dar es Salaam na Pwani kushiriki katika uzinduzi huo. Taarifa ya Katibu Mkuu wa klabu ya Msasani Jogging ndugu Mangula inatanabaisha zaidi.
Katibu Mkuu wa Msasani Jogging Bwana Mangula akichangia harambee Kunduchi
Akizungumza na mwandishi wa blogu hii Bwana Mangula alieleza kwamba katika uzinduzi huo klabu takriban20 zimealikwa na kuthibitisha kushiriki na kuzitaja klabu hizo kuwa ni Biafra, Namanga, Barafu, Mzimuni, Kata 14, Kongowe, Timberland, Kawe Jogging, Kawe Beach, Ukwamani, Unga unga Jogging ya Kawe, Kunduchi Kwanza Jogging, Kunduchi Jogging, Fanja Jogging ya Msasani, Msufini Jogging na Dovya Jogging
 


Bwana Mangula alifafanua zaidi kwamba, uzinduzi huo utatanguliwa na mbio za pole pole zitakazowashirikia wanamichezo wote na zitaanzia maeneo ya CCBRT Msasani kuelekea Namanga hadi Mbuyuni kuelekea kanisa la mtakatifu Petro hadi shule ya msingi Oysterbay, mbio zitaendelea hadi katika fukwe za Coco kuelekea barabara ya Chole hadi Msasani Mwisho barabara ya kuelekea soko la samaki la msasani na kuishia katika fukwe za Msasani ambapo michezo mbalimbali ya ufukweni itafanyika na baadaye wanamichezo wote watajumuika pamoja katika uzinduzi rasmi

Pia, alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wadau na wanamichezo wote. 




No comments:

Post a Comment