Wednesday, December 03, 2014

BIAFRA YASHIRIKI KATIKA SHEREHE ZA KUKABIDHI VYETI GYA USAJILI KWA VILABU VYA JOGGING TEMEKE TARE 30 NOVEMBA, 2014

Katika kuhakikisha tasnia ya mchezo wa mbio za pole pole inakuwa rasmi na kutambulika, Chama cha Mchezo wa Mbio za Pole wilaya ya Temeke (TEJA) kiliandaa hafla fupi ya kukabidhi rasmi vyeti vya usajili kwa vilabu 8 vinavyojihusisha na mchezo wa mbio za polepole wilayani Temeke.

Baadhi ya wanajogging katika sherehe hizo

Mwenyekiti wa klabu ya michezo ya Biafra ndugu Abdul Mollel akiwasalimia wanamichezo
 
Makamu Mwenyekiti wa TEJA ndugu Jimmy Mkande
Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa ni Mheshimiwa Abdullah Ally Hassan Mwinyi ambaye ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki akiiwakilisha Tanzania.
Mgeni rasmi katika ubora wake sambamba na wanamichezo
Mgeni rasmi alipata wasaa wa kusikiliza risala iliyosomwa kwake na waandaaji wa sherehe hizo kabla ya kuanza kwa zoezi la ugawaji wa vyeti ambapo katika majibu yake aliwashauri waandaaji kuandaa sherehe nyingine ambapo yale ambayo yameombwa na vikundi kupitia risala yao yatatolewa taarifa ya utekelezaji.
Risala ikisomwa kwa mgeni rasmi



Mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo la ugawaji vyeti burudani mbalimbali ziliendelea katika kuisherehesha siku yenyewe. 
Mgeni rasmi katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na wanachama wa vilabu vya jogging 

Jimmy Mkande akiwa pamoja na baadhi ya wanabiafra

Baadhi ya Wanabiafra katika picha ya pamoja

Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Michezo ya Michezo ya Biafra, tunapenda kuchukua fursa hii kuwapongeza sana viongozi wa Chama cha Jogging aTemeke (TEJA) kwa jitahada zao za kuuimarisha na kuurasimisha mchezo wa mbio za polepole Tanzania. 

No comments:

Post a Comment