Thursday, December 22, 2011

BIAFRA SPORTS CLUB YATOA POLE KWA WAKAZI WA DAR ES SALAAM BAADA YA KUKUMBWA NA MAFURIKO YALIYOTOKANA NA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA

Klabu ya michezo ya Biafra, inatoa pole kwa wakaazi wote wa Dar es Salaam ambao kwa namna moja au nyingine wameathirika na mafuriko ambayo yamesababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha kwa siku ya tatu mfululizo Dar es Salaam na mikoa ya jirani ambayo kwa kiasi kikubwa imepakana na bahari ya Hindi.
 Hapa ni maeneo ya Kinondoni B bondeni kama unaelekea Msisiri

 Bwawa likiwa limefurika na kuingiza maji katika nyumba zinazolizunguka maeneo ya Msisiri
 
Kwa mujibu wa Wakala/Idara ya Hali ya Hewa mvua bado zitaendelea kunyesha na kuleta madhara zaidi. Hivyo, ni wajibu wa wananchi wote kuchukua tahadhari mapema ili kujiepusha na madhara zaidi lakini pia hatuna budi kuwasaidia wenzetu wameathirika na mafuriko haya huku wengine wakikosa makazi, chakula, mavazi na huduma muhimu za kijamii. Mpaka sasa vituo vinavyopokea watu walioathirika na mafuriko haya Shule ya sekondari ya Azania, Shule ya msingi Gilman Rutihinda Kigogo na kwa misaada ya kibinadamu unaweza kupeleka maeneo hayo pia.

 
 
     Inavyoonekana , bado mvua zitaendelea kunyesha hadi jumapili tarehe 25 Disemba, 2011 ambayo itakuwa ni siku ya kusherehekea sikukuu ya x-mass. Unaweza kutembelea blogu ya Muhidini Sufiani, Muhiddini Michuzi, Issa Michuzi, Maggid Mjengwa, John Badi na nyinginezo ili ujionee athari za mafuriko hayo kwa upana zaidi.
           
                                MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA

Thursday, December 15, 2011

HAFLA YA SHUKRANI KWA WANAMICHEZO WOTE WALIOJITOLEA KATIKA KUFANIKISHA ZOEZI LA KUFANYA USAFI HOSPITALI YA MWANANYAMALA TAREHE 9 DISEMBA KATIKA PICHA

Baada ya kumaliza kazi ya kufanya usafi hospitalini pamoja na kugawa misaada kama ilivyopangwa, wanamichezo wote walirejea makao makuu ya klabu ya Biafra ambapo kulikuwa na hafla maalumu ya kutoa vyeti kwa wahisani, pamoja na klabu zote zilizoshiriki katika kufanikisha maadhimisho hayo. Mgeni wa heshima kwenye hafla hiyo alikuwa ni Mzee Faustin Makima ambaye ni mwenyeketi wa serikali ya mtaa wa balozi msolomi yalipo makao makuu ya klabu ya Biafra.
Wanamichezo wakicheza kwaito kabla ya kuanza kwa zoezi la utoaji wa vyeti
 Kwa niaba ya kampuni ya Esoshi General Trading Ltd, ambayo ilitoa paketi mia tano za maziwa ya Tanga Fresh, cheti kilipokelewa na Henry Byarugaba anayeonekana pichani hapo chini.


Mzee Kodi Siara almaarufu Serikali akipokea cheti kwa niaba ya kampuni ya TKT Ltd ambao walijitolea chupa zaidi ya mia tatu za maji ya uhai ya lita moja pamoja na biskuti ambazo ziligawiwa kwa watoto waliolazwa kwenye wodi ya watoto katika hospitali ya mwananyamala

Robert Mwakibugi akipokea cheti kwa niaba ya kampuni ya Promasidor (PTY) Tanzania. kampuni hiyo ilitoa boksi 20 zenye maziwa ya cowbell ya kopo

Bwana Tobias Owur akipokea cheti kwa niaba ya Royal Billy's Lodge ambao walijitolea mchango wa fedha taslimu pamoja fulana 60

Bwana Benson Simba akipokea cheti niaba ya kampuni ya Dabenco Enterprises ambao walijitolea fedha taslimu katika kufanikisha maadhimisho hayo

Bi. Asha M. Warisanga almaarufu mama Kenisha akipokea cheti kwa niaba ya Ninenty Degrees Pub ambayo ndio makao makuu ya klabu ya Biafra. Picha ya chini akikionesha cheti hicho kwa wanamichezo waliohudhuria hafla hiyo
 Bi. Asia Mohamed ambaye ni mwenyekiti wa klabu ya Kunduchi Kwanza akipokea cheti kwa niaba ya Klabu ya Kunduchi Kwanza ambayo ni miongoni mwa klabu zilizofanikisha kazi hiyo.
Bwana Olest Kalembo (Makamu mwenyekiti wa klabu ya namanga) akipokea cheti kwa niaba ya klabu ya Namanga ambayo ni moja klabu kongwe zinazohamasisha mbio za pole pole katika wilaya ya Kinondoni. Klabu hiyo pia ni miongoni mwa klabu zilizofanikisha zoezi hilo.
Bwana Betwely Kyando (katibu mkuu msaidizi wa klabu ya Biafra) akipokea cheti kwa niaba ya klabu ya Biafra
Mgeni wa Heshima mzee Faustin Makima (mwenye kofia) akiwa pamoja na viongozi wa klabu za Namanga na Kunduchi Kwanza pamoja na Biafra mara baada ya kumaliza zoezi la utoaji wa vyeti

Baada ya kumaliza zoezi la utoaji wa vyeti wadau waliendelea kujipatia vinywaji, chakula na burudani mbalimbali hasa muziki



ZOEZI LA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA NA KUGAWA MISAADA KATIKA HOSPITALI YA MWANANYAMALA TARE 9 DISEMBA, 2011 LAFANIKIWA KWA KIASI KIKUBWA

Klabu za michezo za Biafra, Namanga na Kunduchi Kwanza, katika kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru (1961 - 2011) ziliazimia kufanya usafi wa mazingira pamoja na kugawa misaada kwa wagonjw katika Hospitali ya Mwananyamala ambayo ni hospitali ya Wilaya Kinondoni. 

Wanamichezo pamoja na wadau wengine wote kutoka Kunduchi, Namanga na maeneo tofauti tofauti ya jiji la Dar es Salaam walianza kuwasili katika viwanja vya Biafra - Kinondoni kuanzia saa 12:30 asubuhi kwa ajili ya kugawiwa fulana zenye ujumbe mahususi kwa ajilia ya siku hiyo pamoja na maandalizi ya kuanza mbio za pole pole (jogging) kuelekea sehemu ya tukio - hospitali ya Mwananyamala.
Kama inavyoonekana pichani, msafara wa wanamchezo uliwasili katika hospitali ya Mwananyamala mnamo majira ya saa 1:20 asubuhi

Ili kuondoa usumbufu wa kelele kwa wagonjwa katika hospitali ya Mwananyamala, wanamichezo waliingia hospitali kwa mbio za pole pole kimya kimya (Picha kwa hisani ya Blogu ya John Badi)

Mara tu baada ya kuwasili lilifuatia zoezi la kugawana vufaa vya kufanyia usafi na majukumu mengine. Pichani ni mwanahabari mkongwe John Badi  (mwenye kamera) pamoja na dada Asia Mo'hd (mwenyekiti wa Kunduchi Kwanza Sports Club na Bw. Tobias Owur (mkurugenzi wa Royal Billy's Lodge)

Zoezi la kufanya usafi wa mazingira likaanza moja kwa moja kama wanavyoshuhudiwa wanamichezo wakizoa taka


Mwanabiafra Robert Mwakibugi hakuwa nyuma katika kuhakikisha shughuli inafanyika kwa ufanisi zaidi, hapa anaonekana akiweka 'gloves'zake vizuri tayari kuingia kazini

Mwanabiafra Robert Mwakibugi kiwakilisha maziwa ya cowbell yaliyotolewa na kampuni ya Promasidor kwa watoto waliolazwa kwenye hospitali ya Mwananyamala 
Viongozi wa klabu za Biafra na Kunduchi wakikabidhi sehemu ya msaada kwa viongozi wa hospitali
Katibu wa hospitali ya Mwananyamala akipokea sehemu ya paketi 500 za maziwa ya tanga Fresh kwa ajili ya kugawa kwa wagonjwa hospitalini hapo
Baadhi ya wasanii wa bendi ya mapacha watatu wakiongozwa na Khalid Chokoraa wakikabidhi maziwa ya Tanga Fresh kwa Katibu wa Hospitali ya Mwananyamala

Khalid Chokoraa akigawa maziwa ya cowbell kwa wazazi katika wodi ya wazazi

Wadau wakiwajulia hali wagonjwa hospitalini

Mwanabiafra mzee Faustin Makima akimkabidhi mmoja wa wagonjwa mche wa sabuni
Mweka hazina wa klabu ya Namanga Michael J almaarufu Mopao akimkabidhi maziwa ya Cowbell moja wa wazazi aliyejifungua wakati wa mkesha wa maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru

Mwenyekiti wa klabu Kunduchi Kwanza Asia Moh'd akimpa biskuti mtoto aliyelazwa hospitalini hapo kutokana na majeraha ya kuungua moto

Pichani ni dada katibu msaidizi wa Klabu ya Namanga (mwenye suruali nyeusi) na Bi. Everlast wakiendelea na usafi


Akiwakilisha klabu ya Namanga mzee Ibrahim Lincoln almaarufu 'Mjomba'
Wadau wengine walikumbushi enzi kwa kukamata mpini wa jembe na kulima kama wanavyoonekana pichani

Mwanabiafra  Mustafa Muro akifyeka majani

Wanamichezo wakijadiliana

Pichani kutoka kushoto ni Angel, Happy Mdeka na Khamis S. almaarufu Masharubu


 

Wengine walifanya usafi huku wakicheza muziki na tabasamu la hali ya juu kama wanavyoonekana pichani wanamichezo hawa

Mwimbishaji maarufu wa klabu ya Namanga almaarufu Likopa akionesha kipaji cha mchezo wa sarakasi mara baada ya kumaliza zoezi la kufanya usafi hospitalini hapo

Wanamichezo wengine walichangia damu kwa wagonjwa hospitalini hapo kama anavyoonekana Mama Kenisha mara baada ya kutoa damu akiwa pamoja na wanamichezo wengine

Baada ya kumaliza kazi ya kufanya usafi hospitalini pamoja na kugawa misaada kama ilivyopangwa, wanamichezo wote walirejea makao makuu ya klabu ya Biafra ambapo kulikuwa na burudani kadha wa kadha na likafuatiwa na zoezi la utoaji wa vyeti kwa wahisani, pamoja na klabu zote zilizoshiriki.



Tuesday, December 06, 2011

HARAMBEE YA KUCHANGISHA FEDHA KWA AJILI YA KUFANIKISHA SHUGHULI YA KUFANYA USAFI NA KUTOA MISAADA KWA WAGONJWA KATIKA HOSPITALI YA MWANANYAMALA YAFANA SANA

Siku ya Jumapili, tarehe 4 Disemba, 2011 katika hafla ya uzinduzi wa Royal Billy's Lodge ambayo ipo nyuma ya Kanisa KKKT Tangi-Bovu palifanyika pia harambee kwa ajili ya kuchangia shughuli ya kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Mwananyamala pamoja na kutoa misaada ya hali na mali kwa wagonjwa katika wodi ya wazazi na wodi ya watoto hospitalini hapo. Kabla ya kuanza kwa hafla ya uzinduzi wa lodge hiyo na harambee, wakimbiaji wa mbio za pole pole (jogging) kutoka vilabu vya Biafra, Namanga, Kunduchi, Mbezi Beach, Temeke na wenyeji Tangi Bovu walikimbia mbio hizo kutoka Tangi Bovu kupitia Kawe na kurudi Tangi Bovu.
 Baada ya mbio za pole pole kumalizika wakimbiaji waliendelea kufanya mazoezi kwa mtindo wa aerobics na kama kawaida ili aerobics inoge basi unapigwa muziki na kaka Michael J almaarufu Mopao anaongoza mazoezi hayo

 Mmoja wa wakurugenzi wa Royal Billy's Lodge ndugu Tobias Owur akiingia wa mwisho baada mbio za pole pole - wakimbiaji wengi hawakumaliza mbio kwa kukimbi kama zilivyoanza.

 Wana-jogging wengine walifikia vitini kama anavyoonekana kaka Mustafa Muro

 Kutoka Kushoto ni Mama Kenisha Mkurugenzi wa Biafra Sports Club, Tobias Owur mmoja wa wakrugenzi wa Royal Billy's Lodge na Abdul A. Mollel Mwenyekiti wa Biafra Sports Club

 wana-jogging wengine waliona viatu ni vizito na havivaliki tena

 Dada Edita wa Namanga Jogging akinyoosha kiuno baada ya mbio

 Wakiwakilisha Biafra - Kutoka kushoto Jacqueline Mugalura, Yahya Poli na Ally Masharubu
 Mbusilo Joseph - katibu wa Kunduchi Kwanza pamoja na KP wa Temeke Jogging

 Noah Machaka wa Biafra

 Baada ya kumaliza mbio na burudani za hapa na pale, wana-jogging waliingia ukumbini kwa ajili ya kuanza harambee. Ndugu David Mwaka ambaye ni Mwenyekiti wa Namaga Jogging na Mkurugenzi wa Esoshi General Trading akiwakaribisha wageni ukumbini

 Katibu wa kamati ya maandalizi akiweka mambo ya teknolojia sawa sawa akiwa sambamba a mhamasishaji wa kamati toka klabu ya namanga Charles Juma

Mdau Henry Byarugaba akiingia ukumbini, yeye pamoja na mchango wa fedha ameongeza pakiti 100 za maziwa ya Tanga Fresh toka kwenye idadi ya awali ambayo 400 hivyo kufikisha idadi ya pakiti 500

 Mhamasishaji wa kamati Charles Juma alipigishwa magoti na kugombolewa ambapo pesa iliyopatikana iliongezewa kwenye mahitaji ya kukamilisha shughuli hiyo.

 Bwana Benson Simba akiwasilisha ahadi ya Royal Billy's Lodge na Dabenco Enterprises ambao wamechangia fedha taslimu pamoja na fulana kwa ajili kuvaliwa siku hiyo.

 Tobias Owur Almaarufu mkenya (mwenye miwani) akiwasilisha mchango wake

 Mama Kenisha akipiga makofi baada ya kuahidi kuchangia fedha tasilimu pamoja na katoni kadhaa za sabuni

 Mama Kenisha na Tobias Owur wakisoma ujumbe mfupi wa maandishi toka kwa wadau walio nje ya ukumbi ambao nao wameahidi kuchangia zoezi hilo

 Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi Abdul Mollel sehemu ya fedha zilizokusanywa papo hapo kwenye harambee

 Baada ya harambee kumalizika na Charles kugombolewa ilikuwa ni vicheko na furaha tele kama wanavyoonekana mama Kenisha, Mopao na Charles mwenyewe wakicheka kwa furaha

 Katibu wa kamati ya Maandalizi akiteta na wadau mbalimbali
 Meza iliwakilishwa na Mollel ndugu Joseph Mwaka (katikati) na Mjomba Ole

 Katika picha ya pamoja ni wana-jogging