Wednesday, November 28, 2012

BONANZA LA MICHEZO NA BURUDANI LAWAKUTANISHA WADAU MBALIMBALI TAR 17 NOVEMBA, 2012

Jumamosi tarehe 17 Novemba, 2012 wanamichezo kutoka katika klabu mbalimbali za jogging pamoja na wadau wengine walikutana katika Bonanza lilioandaliwa na klabu ya michezo ya Biafra. Bonanza hilo lililopambwa na Serengeti Breweries kupitia bia ya Serengeti lilihusisha michezo pamoja na Burudani mbalimbali.

Add caption


Wanamichezo walikutana makao makuu ya Biafra, 90 Degrees pub kuanzia saa 12 asubuhi. Mazoezi ya mbio za pole pole kuzunguka maeneo mbalimbali ya manispaa ya Kinondoni, kata ya Mwananyamala zilifanyika punde baada ya vilabu vyote alikwa kufika klabuni.

Wanamichezo toka Mzimuni jogging

Mara baada ya kumaliza mbio za pole pole, wanamichezo walijongea katika viwanja vya Biafra kwa michezo mbalimbali ikiwemo mechi ya soka la veterani kati ya Care Veterani na kombaini ya vilabu vya jogging.

Care Veterani
Mchezaji wa Care Veterani Said Babaa akijiandaa kupatiwa huduma ya kwanza

Ayoub Layson wa Biafra akiongoza katika mashindano ya kutembea na yai kwenye kijiko
Michezo ni furaha
 Baada ya michezo mbalimbali wanamichezo pamoja na wadau wengine walirejea klabuni ambapo burudani mbalimbali zilikuwa zikiendelea. Hatimaye ukafika wakati ambapo baadhi ya vilabu vilitoa zawadi kwa timu ya soka ya vijana ya Biafra ambapo klabu ya Seamens ya Kigamboni walitoa mpira halisi kwa timu hiyo.

Katibu Mkuu wa Seamen Club Kaka Elly akimkabidhi zawadi ya mpira Katibu Mkuu wa Biafra Yahya Poli

Katibu Mkuu wa Biafra akiuonesha mpira kwa washiriki wa Bonanza

Katibu Mkuu wa Biafra akishangilia zawadi ya mpira pamoja na Wana-Seamen

Baada ya kuguswa na zawadi ya mpira iliyotolewa na Seamen Club kwa timu ya vijana ya Biafra, Magogoni Veterani nao walichangia pesa taslimu Sh. 5000/= kwa ajili ya mfuko wa timu hiyo. 
Magogoni Vetrani wakijinadi

Kwa mbwembwe na adabu wakiwakilisha mchango kwa mweka hazina wa Biafra Bi. Asha M. W.

Baada ya matukio hayo mahususi wanamichezo waliendelea kupata burudani mbalimbali zilizoandaliwa kwenye bonanza hilo ikiwemo promosheni ya bia ya serengeti. 
Kilinge cha wana Seamen club

Kilinge cha Kunduchi Kwanza

Kilinge cha wanabiafra

Kilinge cha Namanga Sports Club

Kaka Mudi toka Temeke Jogging akiwaimbisha wanamichezo

Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel (kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa kamati ya nidhamu ya Biafra Mustafa Muro (kulia)
Ummy wa Kunduchi Jogging (aliyesimama) akifuatilia jambo na Mwenyekiti wa Kunduchi Kwanza Asia Mohamed (mwenye shati la draft)