Friday, April 12, 2013

WANABIAFRA WAAZIMIA KUSHIRIKI KATIKA MAFUNZO MBALIMBALI

Wanachama wa klabu ya michezo ya Biafra walikutana katika ukumbi wa 90 Degrees Pub kwa ajili ya mkutano wa kawaida ambapo ajenda kuu ya mkutano huo ilikuwa ni kubaini mahitaji ya mafunzo mbalimbali kwa wanachama wake. Akifungua mkutano huo, Makamu Mwenyekiti wa klagbu hiyo Bi. Jaqueline Barozi (pichani chini) aliwakumbusha wanachama zaidi ya 22 waliohudhuria kikao hicho kuwa jitihada za kutoa mafunzo zina lengo kuwapa fursa wanachama kupata maarifa katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo kwa kadri ya mapenzi yao.
Pia akizungumza katika kikao hicho, katibu mkuu ndugu Yahya Poli aliwakumbusha wadau kuwa kwa mujibu wa Mpango wa Utekelezaji wa Malengo ya Klabu (MUMK) pamoja na Mpango Kazi wa mwaka 2013 klabu imedhamiria kutoa fursa za mafunzo mbalimbali yakiwemo masuala ya ujasiriamali kwa wanachama wake ili waweze kutimiza ndoto na malengo yao ya kujikwamua kiuchumi. 
  
Mara baada ya kikao hicho wanachama waliohudhuria waligawiwa fomu za Kubaini Mahitaji ya Mafunzo kwa Wanachama ili wazijaze na kuzirejesha kwa ajili ya utekelezaji. Kama ungependa kujiunga katika mpango huu wa mafunzo kwa wanachama wa klabu ya michezo ya Biafra, bofya kiunganishi cha "downoload" hapo chini kisha uijaze na kuituma fomu hiyo kwa katibu mkuu katika anuani zinazoonekana kwenye fomu hiyo.

No comments:

Post a Comment