Tuesday, April 09, 2013

UZINDUZI WA KLABU YA MSASANI JOGGING TAREHE 7 APRILI WAFANA

Kama ilivyotolewa taarifa awali, uzunduzi wa klabu ya Msasani Joggiging ulifanyika jumapili tarehe 7 Aprili, 2013 kama ilivyopangwa. Mgeni rasmi katiak uzinduzi alikuwa ni Makamu wa Rais wa Shrikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania ndugu Phares Magesa ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM. Pia uzinduzi huo uliohudhuriwa na wanamichezo zaidi ya mia nane kutoka katika vilabu vya jogging zaidi ya 20, ulihudhuriwa pia na Diwani wa Msasani (viti maalum) Mheshimiwa Christina Kirigiti.

Msasani Jogging wakiongoza Jogging
Baadhi ya klabu zilizoshiriki uzinduzi huo ni Biafra, Namanga, Kunduchi Kwanza, Msufini, Family Jogging, Kawe Social & Sports Club, Kawe Beach Jogging, Kunduchi Jogging, Sotojo, Ukwamani Jogging, Barafu, Mzimuni, Kata 14, Kongowe, Timberland,Unga unga Jogging, Fanja Jogging, Dovya Jogging, n.k. Pichani chini ni baadhi ya vilabu vilivyoshiriki uzinduzi huo vikiwa kwenye jogging.






Mara baada ya jogging iliyokuwa ya takriban kilomita 10 na kuishia katika fukwe za msasani, wanamichezo wote waliendelea mazoezi ya aerobics yaliyokuwa yakiongozwa na ndugu Michael Juma maarufu Mopao kama wanavyoonekana pichani chini.
Punde mgeni rasmi aliwasili eneo la tukio na kupokelewa na Mwenyekiti wa Msasani Jogging ambaye aliambatana na Katibu Mkuu wa Chama cha Jogging Kinondoni ndugu Yahya Poli
Kutoka kulia; Mgeni Rasmi Phares Magesa, M/kiti Msasani Jogging na Katibu Mkuu Yahya Poli
Katika hotuba yake ya uzinduzi huo, mgeni rasmi aliwaasa wanamichezo kutumia pia fursa zinazowaunganisha pamoja katika michezo kwa ajili ya kujiletea maendeleo ya kiuchumi  na kwa kuonesha mfano alichangia shilingi laki tatu kwenye mfuko wa Msasani Jogging Club ili waweze kuanzisha biashara na wadau mbalimbali walioshiriki uzinduzi huo nao walichangia.
Mgeni rasmi Phares Magesa akiwahutubia wanamichezo
Uzinduzi huo pia uliambatana na burudani mbalimbali ambapo wanamichezo walipata fursa ya kujumuika na kuburudika pamoja. 

Klabu ya Michezo ya Biafra inatoa pongezi kwa wanachama wote wa Msasani Jogging kwa kufanikisha uzinduzi wa klabu yao na kuwasisitiza kuimarisha yao kwa kufuata malengo yaliyopelekea kuanzishwa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment