Friday, April 12, 2013

NI UJERUMANI DHIDI YA HISPANIA KATIKA NUSU FAINALI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

Hatimaye nusu fainali ya ligi ya mabingwa ulaya 2013 itazikutanisha timu bora kabisa toka nchini ujerumani na spain. Droo ya nusu fainali hiyo imefanyika leo huko Nyon nchini Uswisi ambapo imedhihirika kuwa vinara wa ligi ya Ujerumani Bayern Munich ambao wanaongoza Bundesliga kwa pointi 75 watamenyana na FC Barcelona wanaoongoza La Liga kwa pointi 78 wakati Borussia Dortmund inayoshika nafasi ya pili Bundesliga ikiwa na pointi 55 itakwaana na Real Madrid ambayo inashika nafasi ya pili pia kwenye La Liga ikiwa na pointi 65.

Mechi ya kwanza katika kinyan'ganyiro hicho itachezwa katika dimba la Allianz Arena nchini Ujerumani ambapo Bayern Munich itawakaribisha FC Barcelona tarehe 23 Aprili, 2013  na siku inayofuata yaani tarehe 24 Aprili, 2013 katika dimba la BVB Stadion Dortmund, Borussia Dortmund itawakaribisha Real Madrid.

Mzunguko wa pili utachezwa tarehe 30 Aprili, 2013 katika uwanja wa Santiago Bernabeu ambapo Real Madrid itaikaribisha  Borussia Dortmund na tarehe 1 May, 2013 katika uwanja wa Camp Nou Barcelona itachuana vikali na Bayern Munich.



Wadau mbalimbali wa soka nchini Tanzania wameanza kubashiri timu zitakazokutana katika fainali ambapo katika ukurasa wake wa Facebook, mwandishi na mchambuzi mahiri wa michezo nchini hususani mchezo wa soka ndugu Shaffih Dauda ambaye pia ni mtangazaji wa kipindi cha michezo cha redio ya Clouds ameandika hivi: - 
 

 Wachezaji wa Timu ya Vijana ya Biafra (BYFT) nao wamebashiri hivyo hivyo katika ukurasa wao wa Facebook ambapo wanatabiri kwamba itaongezeka mechi nyingine ya watani jadi toka nchini hispania (El Classico) kwa mwaka 2013. 
 
Haya, sisi yetu macho, tunasubiri kipute hicho hadi fainali itakayopigwa katika dimba la Wmbley nchini Uingereza.

 

No comments:

Post a Comment