Sunday, April 14, 2013

BIAFRA YAANZA MCHAKATO WA KUANZISHA TIMU YA MPIRA WA PETE

Idara ya wanawake katika Klabu ya Michezo ya Biafra inawahamasisha na kuwaalika wasichana na wanawake wenye vipaji vya mchezo wa mpira wa pete (Netball) na mpira wa miguu kujiunga na klabu na kisha kuanzisha timu. Akizungumza na blogu hii mmoja wa waratibu wa zoezi hilo Bi. Aziza Mwaimu (pichani chini) alibainisha kuwa miongoni mwa wanachama wa klabu hiyo kuna ambao wanapenda kushiriki michezo ya aina mbalimbali hivyo fursa ya kuanzisha timu ni ya kipekee kwao kushiriki michezo
Aziza Mwaimu akionesha kipaji cha kupiga danadana
Makamu M/Kiti wa Biafra Jaqueline Barozi (kulia) akikokota mpira
Kama unapenda kujiunga na timu ya wanawake ya Biafra wasiliana na Katibu Mkuu kwa anuani inayoonekana kwenye kiunganishi upande wa kulia wa blogu hii.

No comments:

Post a Comment