Thursday, April 18, 2013

BLOGU YA BIAFRA YATEMBELEWA ZAIDI YA MARA 600 KWA MWEZI MACHI NA APRILI, 2013

Klabu ya michezo ya Biafra  inatoa shukrani kwa watu wote kutoka mataifa mbalimbali duniani kwa kutembelea blogu yake. Katika kipindi cha mwezi mmoja tangu tarehe 20 Machi hadi leo 18 Aprili, 2013 imetembelewa zaidi ya mara 600 na watu kutoka Tanzania, Marekani, Urusi, Uingereza, Oman, Ujerumani, Ufaransa, Brazili, China na Sweden.
Takwimu za leo

Akizungumzia takwimu hizo, Katibu Mkuu wa klabu hiyo ndugu Yahya Poli alibainisha zaidi kwamba blogu hiyo imetembelewa zaidi ya mara 8000 tangu kuanzishwa kwake na pia alitoa wito kwa makampuni na wafanyabiashara kutumia blogu hiyo kutangaza bidhaa zao.

No comments:

Post a Comment