Thursday, April 11, 2013

TAIFA JOGGING YABADILI JINA ILI KUKIDHI MATAKWA YA USAJILI WA KLABU YAO.

Klabu ya michezo ya Taifa Jogging imebadili jina lake kwa mujibu wa ushauri wa msajili wa vyama na vilabu vya michezo Tanzania. Ushauri huo umetokana na klabu hiyo kuwa katika mchakato wa kupata usajili rasmi toka katika Baraza la Michezo Tanzania (BMT). Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Mlezi (Patron) wa klabu hiyo bwana Mustafa Mgawe (pichani chini) alisema kwamba kwa sasa klabu hiyo itasajiliwa kwa jina la FAITA JOGGING. Aliendelea kueleza kuwa mchakato wa usajili tayari umeshaanza na unaendelea vizuri.
Viongozi waandamizi wa FAITA JOGGING kutoka kushoto Mrs. Fuime (Mwenyekiti) na Mustafa Mgawe (Mlezi)
Pia Mlezi huyo alitoa rai kwa vilabu vyote vya jogging kuungana na kufuata nyayo za vilabu vya jogging vya manispaa ya Kinondoni ambavyo vipo katika mchakato wa kuanzisha chama cha jogging katika manispaa hiyo. 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Biafra, ndugu Yahya Poli kwa niaba ya Wanabiafra wote aliwapongeza wana FAITA JOGGING wote kwa ushirikiano walio nao na vilabu vingine na hasa kwa kuanzisha timu ya mpira wa pete (netball) ya wanawake ambayo inajulikana kama FAITA QUEENS. Timu hiyo ilicheza mechi ya kirafiki na timu ya mpira wa pete ya Mzimuni Jogging na kuwafunga.
KIKOSI CHA FAITA QUEENS PICHANI
 

No comments:

Post a Comment