Tuesday, March 26, 2013

MCHAKATO WA MASHINDANO YA FIFA COPA COCA COLA (U15) 2013 WAANZA RASMI

Mchakato wa mashindano ya Fifa Copa Coca Cola kwa mwaka 2013 umeanza rasmi leo ambapo Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodgar Chilla Tenga alifungua semina elekezi iliyoshirikisha makatibu wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa na waratibu wa mikoa wa michezo ya UMISSETA ambao katika ngazi ya wilaya na mkoa wao ndio waendeshaji na wasimamizi wa mashindano hayo. 


Kikosi cha Timu ya Vijana ya Bifra (BYFT) kilichoshiriki michuano ya Copa Coca Cola (17) mwaka 2012 mkoa wa Kinondoni


BYFT wakisalimiana na wachezaji wa African Talent - Copa Coca Cola (U17) 2012
Rais Tenga alitanabaisha kwamba kuanzia mwaka huu, michuano ya FIFA Copa Coca-Cola itakuwa ikishirikisha watoto wenye umri chini ya miaka 15. Hivyo, amewataka viongozi wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kuhakikisha wanaingiza wachezaji wenye umri sahihi katika michuano hiyo. 
Nahodha wa BYFT (kulia) pamoja na mwamuzi na nahodha ya African Talent
Rais Tenga alionya kuwa hakuna jambo la kipuuzi kama kuchomekea wachezaji ambao wamezidi umri unaotakiwa kwa vile lengo la michuano ya aina hiyo ni kubaini vipaji na kuwafanya watoto wapende kucheza mpira wa miguu. Pia alisisitiza washiriki wa semina hiyo kuwepo wakati michuano hiyo ikiendelea “Kwanza nawashukuru kwa kutenga muda wenu na kuhudhuria semina. Lakini ni vizuri pia mkahakikisha mnakuwepo kwenye mashindano ili kutekeleza haya ambayo tutakubaliana katika semina hii. Mkileta mtu mwingine anaweza kutuanzishia mambo mengine badala ya yale tutakayokubaliana,” amesema Tenga.
Baadhi ya wachezaji wa BYFT wakiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Klabu ya Biafra - Michael Silili (mweye fulana ya nyeupe)
 
Michuano hiyo kwa mwaka huu 2013 inatarajiwa kuanzia katika ngazi ya wilaya mwezi Aprili na fainali zake katika ngazi ya taifa zitafanyika mwezi Septemba.  
 
Viongozi, wachezaji na mashabiki wa BYFT katika picha ya pamoja
Klabu ya michezo ya Biafra inatarajia kuingiza timu yake ya vijana katika michuano mara baada ya Kamati ya Utendaji kukutana na kocha, mameneja wa timu pamoja na wachezaji ili kupanga mikakati ya ushiriki wao.

No comments:

Post a Comment