Tuesday, March 12, 2013

UNAALIKWA KUJUMUIKA NA MARAFIKI SIKU YA IJUMAA TAREHE 15 MACHI, 2013

Kama ilivyo ada, kwa mara ya pili tena CHIMBINGA UNIQUE PUB kwa kushirikiana na BIAFRA SPORTS CLUB wanakualika wewe mdau, kujumuika pamoja na marafiki mbalimbali katika shamra shamra za kuianza wikiendi yako. Akizungumza maandalizi ya siku hiyo mdau wa Biafra na Mkurugenzi wa Chimbinga Unique Pub ndugu Robert Mwakibugi (pichani) almaarufu CHIMBINGA alithibitisha kwamba tarehe 15 Machi, 2013 kuanzia saa 1:00 jioni wadau wote watakuwa Chimbinga Unique Pub tayari kwa kuianza wikiendi pamoja na marafiki. 
Robert Mwakibugi akiiwakilisha Chimbinga Unique Pub
 Katika kuipendezesha siku hiyo, Chimbinga alifafanua kuwa kutakuwa na burudani mbalimbali hasa muziki wa bolingo, funk, sweet reggae, n.k. na katika kuinogesha zaidi siku hiyo patakuwa na mbuzi choma (BBQ) kwa ajili ya wadau watakaohudhuria.


Mwanabiafra na mdau maarufu wa Chimbinga Unique Pub - Dastun Barozi (kulia) akiwa na marafiki zake Chimbinga
Ili kuweza kuifanya siku hiyo iwe ya kipekee na ipendeze zaidi, Chimbinga aliwakumbusha wadau kuchangia uchakavu wa Tshs. 10, 000/= kwa kila mtu anayependa kushiriki siku hiyo.

USISAHAU, NI IJUMAA HII TAREHE 15 MACHI, 2013. NJOO WEWE, NA YULE TUKUTANE NA MARAFIKI ZETU WA UKWELI, TUPATE BURUDANI ZA UKWELI NA TUIANZE WIKIENDI YETU KIUKWELI.

No comments:

Post a Comment