Thursday, May 17, 2012

MCHEZAJI NGULI WA ZAMANI YA TIMU YA TAIFA NA YANGA KUTEMBELEA MAZOEZI YA BIAFRA KIDS

Katika harakati za kuwapa fursa za kujifunza toka kwa wachezaji wa mpira wa miguu wa zamani, klabu ya Biafra imeanzisha programu maalumu ya kuwakutanisha wachezaji wa zamani na vijana hao. Programu hiyo inayoitwa 'inspired by the legends' itaanza rasmi juma hili na itafanyika takriban mara mbili kila mwezi.
mchezaji nguli (legend) mwenye bahati ya kufungua programu hiyo ni Edibiliy Jonas Lunyamila (pichani chini) ambapo atatembelea mazoezi ya Biafra Kids siku ya ijumaa tarehe 18, Mei, 2012 katika viwanja vya Biafra Kinondoni.
Edibily Jonas Lunyamila aka Lunya

Akizungumza juu ya ujio huo, kocha wa Biafra Kids William John Masika alieleza kuwa amefanya mawasiliano na mchezajihuyo na amethibitisha kuhudhuria mazoezi na baadaye kuzungumza na vijana hao. Pia atatumia fursa hiyo kutoa ushauri kwa viongozi wa namna ya kuwaendeleza vijana hao kwa kufuata misingi na miiko ya mchezo wa mpira wa miguu.

Kwa niaba ya viongozi, wanachama, wapenzi na mashabiki wa Biafra Sports Club, tnapenda kuchukua fursa hii kumkaribisha Lunyamila klabuni kwetu. Karibu sana!!!!

No comments:

Post a Comment