Friday, May 18, 2012

BIAFRA SPORTS CLUB YAZIKARIBISHA KLABU ZA JOGGING ZA KAWE NA TAIFA KUFANYA JOGGING PAMOJA

Katika kuendeleza uhusiano na ujirani mwema mwema, klabu ya michezo ya Biafra inaendeleza programu yake endelevu ya kufanya mazoezi ya pamoja na klabu mbalimbali za jogging mkoani Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla. Programu hiyo iliyoanza kabla ya klabu kusajiliwa itaendelea tena jumapili ya tarehe 20 Mei, 2012 ambapo klabu ya Taifa Jogging ya Temeke na Kawe Jogging ya Kawe mzimuni watakuwa wageni wa klabu ya Biafra.
Baadhi ya Wana-Kawe jogging

Akithibitisha wa klabu ya Kawe ndugu Lazaro alieleza kuwa ni fursa nzuri kwa wanamichezo kukutana kwa apmoja mara kwa mara na kubadilishana mawazo pamoja na uzoefu wa namna ya kuziendeleza klabu zetu.

Klabu ya Biafra inawakaribisha wakaazi wote wa Kinondoni hasa wapenda mazoezi katika kufanya mazoezi ya pamoja siku hiyo n siku nyingine. 

No comments:

Post a Comment