Wednesday, May 02, 2012

BIAFRA KIDS YAJIANDAA KUIKABILI TIMU YA MCHANGANI FC TAREHE 3 MEI, 2012

Michuano ya Copa Coca Cola kwa vijana walio chini ya umri wa miaka 17 inaendelea tena juma hili ambapo timu ya Biafra Kids inajitupa tena uwanjani tarehe 3 Mei, 2012 kupambana na timu ya mchangani FC ya Mwananyamala. Mchezo huo utafanyika katika uwanja wa Kinondoni Muslim, Dar es Salaam kuanzia saa 10:00 jioni.  


Baadhi ya wachezaji wa Biafra Kids wakipasha misuli kabla ya kuanza mechi siku walipoitungua African Talent magoli 3 - 1 katika uwanja wa Mwl. Nyerere, Makkurumla.

Akiizungumzia mechi hiyo mara baada ya mazoezi makali yaliyofanyika katika fukwe za Coco hapo jana, nahodha wa timu hiyo Hussein Tahiddin (pichani chini) aliwaonya vijana wa Mchangani wajiandae maana wanafanya mazoezi ya nguvu ili kuhakikisha wanashinda mechi hiyo na zilizobaki na hatimaye kuchukua kombe. Aliwashauri pia vijana wenzake waonyeshe vipaji vyao kwa kuwa wasipoangalia kombaini ya timu ya Kinondoni itaundwa na wachezaji wa Bifra Kids peke yao kwa kuwa wao ndio wanaoonyesha kandanda safi kwenye michuano hiyo. 
Hussein Tahiddin - Nahodha wa Biafra Kids 

Kama kawaida yao viongozi, wanachama na mashabiki wa timu ya Biafra Kids, wameahidi kuwaunga mkono vijana hao kwa kwenda kwa wingi uwanjani kuwashangili na kuwapa hamasa ya ushindi. pia waliwatoa wasiwasi wachezaji wote na kuwaasa wazingatie maelekezo ya walimu na viongozi wao ili kujipatia ushindi kwenye mechi hiyo.

MUNGU IBARIKI BIAFRA KIDS


No comments:

Post a Comment