Sunday, May 13, 2012

HALI YA HEWA YASHUSHA IDADI YA WANA-JOGGING JUMAPILI

Hali ya hewa ya mawingu na manyunyu ya hapa na pale imesababisha wana-jogging wengi wasijitokeze kwa ajili ya kufanya mazoezi ya pamoja kama ilivyopangwa leo. Wanamichezo waliojitokeza ni wachache sana kulinganisha na majuma yaliyopita.
Wanabiafra wakiwa barabara ya Leaders kuelekea barabara ya Kinondoni


watoto nao hawako na wala hawaachwi nyuma kwenye 'jogging'


Bila kujali uchache wao, wanabiafra walifanya mazoezi kama ilivyopangwa na hatimaye walimaliza kwa kufanya 'aerobics' klabuni. Mazoezi hayo japo yalifana lakini hali ya mazingira haikuwa nzuri kutokana na eneo kubwa linatumika kufanyia mazoezi hayo kuwa na madimwi ya maji yatokanayo na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanabiafra katika mazoezi ya aerobics wakiongozwa na Noha Machaka


Baada ya kumaliza mazoezi, wanachama waliungana pamoja na moja moja walikwenda katika uwanja wa Mwl. Nyerere, Magomeni Makurumla kuishangilia timu yao ya Biafra Kids ambao walikuwa wakichuana na Vijana Muslim mchezo ambao ulimalizika kwa Biafra Kids kuichabanga bila huruma timu ya Vijana Muslim kwa mabao mawili kwa moja.


No comments:

Post a Comment