Monday, May 07, 2012

MAZOEZI YA 'JOGGING' YAFANA NA KUWAKUTANISHA WANAMICHEZO TOKA KLABU MBALIMBALI KATIKA FUKWE ZA COCO

Jana (jumapili - 04/05/2012) kama kawaida mazoezi ya mbio za pole pole (jogging) yaliendelea kwa Wanabiafra ambapo mbio zilianzia klabuni 90 Degrees kinondoni kupitia Moroko, Kanisa la Mtakatifu Petro, Shule ya Msingi Oysterbay hadi ufukweni Coco.

Wanabiafra wakiwa katika barabara ya Kawawa kuelekea Moroko

Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi Michael Silili akiongoza msafara


Wanabiafra wakiwa barabara ya Ali Hassan Mwinyi Road maeneo ya Oysterbay Police


Mara baada ya kuwasili ufukweni mazoezi ya viungo yaliendelea kwa kutengeneza duara kubwa na mwelekezaji akiwa katikati ya duara hilo.


(m)duara

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Ally Masharubu (mwenye jezi Na. 7) akipasha viungo


(m)duara tena


Kutoka kulia ni Mustafa Murro (mwenyekiti kamati ya Nidhamu na Rufaa), Nancy R Rupia (mjumbe Kamati ya Ufundi) na Jaqueline Barozi (Makamu Mwenyekiti)

Wakati mazoezi yakiendelea ufukweni hapo wana-jogging toka klabu ya Msufini nao waliwasili na moja kwa moja na wao waliendelea na mazoezi ya viungo kama ilivyo ada, na mpiga picha wetu alijongea karibu yao na kusaimiana nao na kisha kuendelea kupata picha mbili tatu.

Wana-Msufini Jogging wakifanya Sit-Ups

Muda si mrefu tena wakaingia wana-jogging wa klabu ya Namanga na kufanya jumla ya klabu tatu tofauti za jogging kukutana ufukweni.

Wana-Namanga Jogging wakitengeneza duara

Wanabiafra wakawaelekeza Namanga namna ya kutengeneza mduara kwa haraka

 Mara baada ya kumaliza mazoezi hayo wana Biafra walirudi klabu na moja kwa moja mazoezi ya aerobics yaliendelea kwa zaidi ya dakika 40. Kama kawaida ili aerobics inoge, muziki ni lazima uchagize na mdundo wa wake ndio unaoongoza mazoezi hayo kama wanavyoonekana wanabiafra wakifurahi mazoezi ya aerobics kwa kufuata midundo ya muziki.


Hii inaitwa washa pikipiki style



Gusa kisigino

Wengine wakaamua kucheza muziki kabisa

Makamu Mwenyekiti (Jaqueline Barozi) na Mwenyekiti (Abdul Mollel)


KARIBU UJIUNGE NA BIAFRA SPORTS CLUB KWA MAZOEZI HAYA YA JOGGING KILA JUMAPILI


No comments:

Post a Comment