Thursday, May 03, 2012

MECHI YA KATI YA BIAFRA KIDS NA MCHANGANI FC YAHAIRISHWA

Chama cha mpira wilaya ya Kinondoni (KIFA) ambacho kina ratibu mashindano ya Copa Coca Cola kwa vijana walio chini ya umri wa miaka 17 kimehairisha tena mechi kati ya Biafra Kids na Mchangani FC iliyokuwa ichezwe leo tarehe 3 Mei, 2012 saa 10 jioni katika uwanja wa Kinondoni Muslim. Kuhairishwa kwa mechi hiyo kunatokana na uwanja huo kujaa yatokanayo na mvua inayoendelea kunyesha katika jiji la Dar es Salaam.

Baadhi ya wachezaji wa Biafra Kids

Uongozi wa KIFA umetanabaisha kuwa unajipanga vyema na mapema iwezekanavyo wataujulisha umma wa wapenda maendeleo ya soka juu ya tarehe na mahali mchezo huo utakapopigwa tena.

Wakati huo huo, viongozi na wachezaji wa timu hiyo wameahidi kuitumia fursa hiyo kuendelea na mazoezi kwa ajili ya kujiweka sawa sawa zaidi kimchezo na kimashindano.

No comments:

Post a Comment