Monday, May 21, 2012

MATUKIO BAADA YA MAZOEZI YA MBIO ZA POLE POLE KATIKA PICHA

Siku ya jumapili tarehe 20 Mei, 2012 klabu ya michezo ya Biafra ilizialika klabu za Taifa Jogging na Kawe Jogging pamoja na wadau wengine katika kufanya mazoezi ya pamoja ya mbio za pole pole 'jogging' ambazo zilianzia katika makao makuu ya klabu ya Biafra kupitia barabara ya Kawawa, Dunga, Peace, Mwin'juma, Kawawa tena na kumalizikia makao makuu ya Biafra.

Wanamichezo wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Taifa Jogging akitoa nasaha zake

Mazoezi hayo yalihudhuriwa na wanamichezo zaidi ya mia moja hamsini kutoka Temeke pamoja na Kinondoni ambapo yaliongeza hamasa hadi kupelekea watu wengine wajumuike pamoja huku nyimbo mbalimbali za kuhamasisha wakimbiaji zikiimbwa kwa ustadi mkubwa.


wanamichezo wakiimba na kucheza klabuni


Baadhi ya viongozi wa Biafra na Taifa jogging

Mashabiki wa soka nao hawakuwa nyuma kuonyesha ushabiki wao kwa kushangilia ushindi wa klabu ya Chelsea ambayo imenyakua ubingwa wa kombe la klabu bingwa ulaya kwa kuitandika sawasawa timu ya byern Munich ya ujerumani kwa mikwaju ya penati.

Wanabiafra Michael Silili (wa kwanza kulia) na Editha Tungara (wa mwisho) katika picha ya pamoja na Bi. Arafa nwenzake wakiiwakilisha Taifa Jogging

Hata mashabiki wa Liverpool nao walikuwepo

Mwanabiafra Editha Tungaraza

Ismail Hamad (kushoto) na Michaele Silili (kulia)


Akizungumza baada ya kumaliza mazoezi mwenyekiti wa Taifa Jogging alieleza kuwa wamefurahishwa sana na mwaliko wa kuja kufanya mazoezi ya pamoja kwa kuwa kutembeleana huku kutaimarisha sana uhusiano baina ya klabu rafiki, hivyo alitumia pia fursa hiyo kuwaalika Wanabiafra Temeke na kufanya mazoezi ya pamoja Taifa jogging pamoja na klabu nyingine.

No comments:

Post a Comment