Wednesday, July 10, 2013

TANZIA TANZIA TANZIA

Juma lililopita limekuwa ni la huzuni kwa wanabiafra na tasnia ya mchezo wa mbio za pole pole (jogging) mkoa wa Dar es Salaam kwa ujumla. mwanzo mwa juma tulipokea taarifa ya msiba wa mke wa katibu Mkuu wa Temeke Jogging (Rasmi) ndugu Togocho ambapo mazishi yalifanyika maeneo ya kurasini Mivinjeni. Vilabu kadhaa vya jogging viliendelea kuonesha umoja kwa kushiriki kwenye msiba huo na mingine.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Biafra Henry Maseko (mwenye shati jeupe) akitoa nasaha kwenye msiba wa mke wa ndugu Togocho


Siku ya Jumatano wanachama wa Biafra kundi la watoto Mtoro Elvis na kaka yake Jimmy Elvis (pichani chini)  nao walifiwa ni bibi yao mlezi ambapo mazishi yalifanyika huko Mlandizi mkoa wa Pwani.
Jimmy Elvis

Mtoro akiwa na kocha Willy
Huzuni iliendelea kutamalaki siku ya jumapili tarehe 7 Julai, 2013 ambapo alfajiri ya siku hiyo klabu ya michezo ya Biafra ilimpoteza mwanachama wake mtoto Aboubakar Iddi Maganga ambaye alifariki kwa ajali ya gari iliyotokea Kibaha mkoani Pwani. Taarifa ziliwafikia Wanabiafra wakati wakiwa katika mazoezi asubuhi hiyo toka kwa baba mzazi wa Aboubakar bwana iddi Maganga ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya Utendaji ya Biafra. Mazishi ya marehemu Aboubakar yalifanyika katika makaburi ya Kinondoni siku ya Jumatatu tarehe 8 Julai, 2013. 

Kaburi alimozikwa Aboubakar iddi Maganga
Baadhi ya waombolezaji




Kaka nathan akiiwakilisha Temeke Jogging



Wafiwa; Iddi maganga na mkewe


Waombolezaji


Rose Mwakibugi (mwenye rasta) pamoja na Asia Mohamed (mwenyekiti wa kunduchi kwanza)

Mwenyekiti wa Kopa Original Jogging  Mustapha alikuwepo
Tunamwomba Mwenyezi mungu azilaze roho za marehemu wote mahala pema peponi.

No comments:

Post a Comment