Sunday, July 28, 2013

MAZOEZI YA MCHAKAMCHAKA (JOGGING) YA JUMAPILI TARE 28 JULAI YAWANOGESHA WANABIAFRA

Wanabiafra leo tarehe 28 Julai, 2013 walijitokeza kwa wingi na kushiriki mazoezi ya mbio za pole pole ambayo yalianzia klabuni, mtaa wa Isere, Kinondoni kisha kuingia barabara ya Kawawa hadi kwenye makutano ya barabara ya Kawawa na Kinondoni, kupitia shule ya sekondari ya Muslim, mwembejini, kona ya tazara mpaka kwenye mataa ya salenda kuelekea barabara ya Ali Hassan Mwinyi kuelekea sea view na hadi katika fukwe za Agha Khan ambapo walifanya mazoezi ya viungo kwa jumla na hatimaye kurejea klabuni kwa mchakamchaka kupitia barabara zilezile walizotumia. Fuatilia matukio yote katika picha.
Tukiingia barabara ya Kawawa kutokea klabuni



Watoto wakiimba kwa shangwe na hamasa
Tulipofika maeneo ya Manyanya, tulikutana na klabu ya Kopa Original upande wa pili wa barabara kuelekea Moroko ambapo Katibu Mkuu alijumuika nao kuwaunga mkono na kuwasalimia.

Katibu Mkuu wa Biafra akivuka barabara kuwasalimia Kopa Original Jogging

M/Kiti wa Biafra - Abdul Mollel Akiimbisha

Maeneo ya makaburini tukielekea shule ya sekondari Muslim

Wale wa mwisho mwisho


Waongozaji wetu Ally Juma ambaye pia ni katibu wa kamati ya ufundi ya Biafra (mwenye tracksuit nyekundu) na Khamis Magodoro (mwenye kizibao) wakituongoza kuingi barabara ya Ali Hassan Mwinyi kwenye mataa ya Salendar Bridge

Tukiingia Barabara ya Ali Hassan mwinyi


Tukikatiza maeneo ya Seaview
 Mara
Tukiingia katika fukwe za Agha Khan/Gymkhana
Mduara wa mazoezi ya viungo





Katibu katika vita dhidi ya kitambi
Mara baada ya mazeozi ya viungo ya pamoja na binafsi, tulipata fursa ya kupiga picha ya pamoja ya wanabiafra wote walioshiriki mazeozi kisha safari ya kirudi klabuni ikaanza.


Picha ya pamoja
Safari ya kurudi klabuni

Mollel akiimbisha kwa mzuka

Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Mipango Robert Mwakibugi (mwenye bukta ya bluu akionesha ukakamavu

Tukiwa klabuni baada ya kumaliza mbio
Tunatoa shukrani za dhati kwa jeshi la polisi, idara ya usalama barabarani kwa kuwa wamekuwa wakituonesha ushirikiano wa hali ya juu kila tunapofanya mazoezi ya mbio za pole pole siku za jumapili, mara zote wamekuwa wakituongoza vizuri na kuonesha utayari wa kutusaidia tunapoomba msaada wao.

MAZOEZI NI AFYA, ACHA KUJIACHIA!

No comments:

Post a Comment