Wednesday, July 24, 2013

BIAFRA SPORTS CLUB NA NAMANGA JOGGING WAFANYA MAZOEZI PAMOJA

Kama ilivyo ada, jumapili hii wanabiafra walikutana tena katika mazoezi ya mbio za pole pole (jogging) ambazo zilikutanisha pamoja na marafiki zao wa Namanga Jogging katika fukwe za Coco, Dar es Salaam. Fuatilia matukio ya siku hiyo katika picha.
Wanabiafra waliowahi mapema klabuni wakijiandaa kuondoka



Msafara ukingia barabara ya kuelekea ada estate


Tukiingia barabara ya Best-Bite


Tukiingia barabara ya Ally Hassan Mwinyi kuelekea Namanga


Tlikutana na Vegas Jogging kwenye kona ya kuelekea Namanga wao wakielekea barabara ya A.H.Mwinyi









Tukiingia fukwe za coco

Namanga Jogging wakifanya mazoezi ndani ya Coco Beach wakiongozwa na Michael Juma (Mopao)

Biafra waliungana na Namanga na kuendelea na mazoezi ya ufukweni

Baadhi ya wanabiafra katika picha ya pamoja

Watoto wa Biafra pichani

Katibu akiwa pamoja na watoto

Mwanabiafra Ayoub Layson
Mara baada ya mazoezi ya nguvu ya ufukweni kwa pamoja na wana namanga Jogging tulianza safari ya kurejea kwenye ngome zetu kwa mbio za pole pole.
Tukijipanga tayari kuanza safari ya kurudi baada ya mazoezi ya ufukweni

Wakati sisi tunarudi wengine ndio walikuwa wanaenda

Tukielekea barabara ya CCBRT

Tukishusha kilima cha CCBRT

Tukipandisha kilima cha CCBRT kuelekea barabara ya Namanga

Barabara ya Namanga
Hapa ni karibu kabisa na Leecaz ambako ni makao makuu ya Namanga Jogging na waliishia hapo sisi tukaendelea na safari ya kurudi klabuni

Barabara ya Best-Bite
Tukielekea klabuni

Utamu wa mazoezi ya viungo

Tukiwa kwenye kikao


Mara baada ya mazoezi, katika kikao chetu cha kawaida, tuliamua kwa pamoja kuwa jumapili ya tarehe 28 Julai, tutafanya mazoezi ya mbio za pole pole kuanzia klabuni hadi fukwe za Agha Khan kupitia barabara ya Kinondoni, Salendar na Seaview. Tunawakaribisha wote! 

MAZOEZI NI AFYA, ACHA KUJIACHIA!!!!

No comments:

Post a Comment