Monday, April 23, 2012

TANZIA

Juma lililopita, klabu ya Biafra ilipata taarifa za msiba toka kwa mwanachama wake na mjumbe wa kamati ya Uchumi na Mipango ya klabu Bi. Mariam Sabaje ambaye amefiwa na kaka yake juma lililopita huko mkoani Mbeya. Mipango ya mazishi inafanyika huko huko Mbeya na Bi. Mariam Sabaje amesafiri Ijumaa ili kuhudhuria msiba huo.
Bi. Mariam Sabaje ( mwenye suruali nyeupe) akiwa pamoja na wanachama wa Biafra

Viongozi, wanachama na mashabiki wa Biafra wanatoa pole kwa mwanachama mwenzao pamoja na familia yake kwa ujumla. Tuko pamoja! Kama ilivyo ada, rambirambi zinaendelea kukusanywa ili tumkabidhi mwanachama mwenzetu na kumpa mkono wa pole. 
Bi. Mariam Sabaje akisherehesha klabuni

BWANA AMETOA! BWANA AMETWAA! JINA LAKE LIHIMIDIWE

No comments:

Post a Comment