Friday, April 13, 2012

TANZIA

Katika juma hili klabu inasikitika kutangaza misiba miwili mfululizo. Katika msiba wa kwanza Mweka Hazina wa klabu Bi. Asha Mweke Warisanga (pichani chini) amefiwa na kaka yake huko Nairobi nchini Kenya. Msiba huo ulitokea mwanzo mwa juma hili na kwa sasa Mweka Hazina huyo yuko Nairobi kwa ajili ya kushiriki maziko.
MRS. ASHA M. WARISANGA - MWEKA HAZINA WA BIAFRA SPORTS CLUB

 Pia mnamo majira ya jioni ya tarehe 12 Aprili, 2012 ilitolewa taarifa ya msiba wa baba mzazi wa mwanachama mwingine wa klabu Bi. Upendo Kimaro. Kwa mujibu wa Upendo (pichani chini), Mzee Kimaro amefariki huko Arusha na yeye yuko kwenye maandalizi ya kuhudhuria msiba huo mapema iwezekanavyo.
UPENDO KIMARO
Klabu inatoa pole na kutuma salamu za rambirambi kwa wanachama wake hao pamoja na familia zao kwa ujumla. Tuko pamoja katika kipindi hiki kigumu cha msiba na majonzi makubwa kwa kupoteza ndugu zetu. Tunamuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema azilaze roho za marehemu mahala pema peponi - Amen

BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA, JINA LAKE LIHIMIDIWE

1 comment:

  1. Poleni sana wanabiafra kwa msiba mlioupata na Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi

    ReplyDelete