Thursday, April 26, 2012

BIAFRA KIDS YACHEZA MECHI YA KWANZA YA MICHUANO YA COPA COCACOLA CHINI YA UMRI WA MIAKA 17

Michuano ya kuwania kombe la Copa Cola kwa vijana walio chini ya umri wa miaka 17 imeanza leo ambapo katika uwanja wa Mwl. Nyerere Magomeni Makurumla timu ya soka ya Biafra Kids ilimenyana na timu ya Eleven Boys.
Kikosi cha kwanza cha Biafra Kids - The Juniors

 Katika mchezo huo timu ya Biafra Kids imepoteza kwa kufungwa goli 4 -2 matokeo yaliyipa changamoto timu hiyo kuongeza bidii ya mazoezi na mbinu mbalimbali za kimchezo ambapo imeonekana dhahiri kuwa timu kadhaa zimesajili wachezaji wenye umri wa zaidi ya miaka 17 kama inajielekeza ligi hiyo.

Biafra Kids pamoja na Eleven Boys wakikaguliwa

Hadi mapumziko tumi hizo zilikuwa zimetoka sare ya 1 - 1 ambapo mchezaji machachari wa timu hiyo Jimmy Elvis Juma ndiye aliyeipatia bao la kufutia machozi.

Mfungaji wa goli la Biafra Kids Jimmy E. Juma

Kipindi cha pili kilikuwa kigumu kwa timu ya Biafra Kids ambapo vijana wa Eleven Boys waliongeza mabao mengine mawili na Biafra Kids kupitia kwa mshambuliaji wake hodari Mashaka Masumbwi walijipatia bao la kufutia machozi.
mjumbe wa kamati ya Utendaji, Henry Maseko (kushoto) na Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Michael Silili (kulia) wakiwa na mfungaji wa goli la kufutia machozi, Mashaka Masumbwi (katikati)

Wakizungumza baada ya kumalizika kwa mechi hiyo, viongozi, wanachama na mashabiki wa klabu ya michezo ya Biafra walionyesha kuridhishwa na kiwango cha wachezaji kwenye mechi hiyo na pia walipata fursa ya kutoa nasaha zao kwa wachezaji, viongozi na hata mashabiki kwa ujumla. Makamu Mwenyekiti wa klabu Bi. Jackline M. Barozi aliwaahidi vijana hao klabu itawasapoti katika kila hatua na kuwasihi waongeze bidii ili mechi zijazo zote tushinde na hatimaye kuchukua kombe.

Baadhi ya wachezaji wa Biafra Kids wakiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya ufundi
Baada ya kupokea nasaha vijana waliahidi kufanyia marekebisho makosa yote yaliyobainishwa na kuwahakikishia wanachama kwamba kombe hili la kopa coca cola litabaki mikononi mwao. Pia walibainisha mahitaji muhimu ili kuweza kukamilisha ndoto yao ya kucheza soka na miongoni mwa mahitaji hayo ni vifaa vya michezo kama vile jezi kwa ajili ya mechi na mazoezi, koni, viatu, soksi, n.k.

Kikosi cha Biafra Kids kilichocheza leo katika picha ya pamoja na mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Michael Silili (wa kwanza kushoto waliosimama) na mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Henry Maseko (wa mwisho kulia waliosimama)

Timu hiyo inajitupa tena katika uwanja wa Mwl. Nyerere, Magomeni Makurumla, jumapili tarehe 29, Aprili 2012 saa 10:00 jioni kuchuana na timu ya African Talent hivyo wamewaomba viongozi, mashabiki na wanachama kuwaunga mkono kwa kuwapatia vifaa vya michezo na kwenda kwa wingi kweny mechi kuwashangilia na kuwapa hamasa ya ushindi.

No comments:

Post a Comment