Friday, April 06, 2012

MWANABIAFRA FURAHA NGANDA KUZIPIGA DAR LIVE TAREHE 8 APRILI, 2012

Kwa wapenzi na mashabiki wa mchezo wa ndondi aka ngumi, aka masumbwi aka mtifuano basi jumapili hii ya tarehe 8 Aprili, 2012 kuanzia saa 10 jioni basi tusikose kwenda kumshuhudia mwanamasumbwi machachari Furaha Nganda (pichani chini) atakapopanda ulingoni kuwawakilisha vyema wanabiafra apmoja na wakaazi wote wa Kinondoni atakapomchakaza mwanadada Jamhuri Said  katika ukumbi wa Dar Live Mbagala. Akizungumzia mpambano huo Furaha alikuwa na haya ya kusema "nawasisitiza wanakinondoni mje kwa wingi kunshangilia maana nakwenda kufanya kazi na si vinginevyo. Nahitaji raudni tatu tu kuangaza ushindi maana 'KO' ndio kitu ninachokifahamu."

FURAHA NGANDA

1 comment: