Thursday, April 12, 2012

KAMATI MBALIMBALI ZA KLABU ZAKUTANA KUJADILI UTEKELEZAJIA WA MAJUKU YA KAMATI HIZO

Kuanzia siku ya Jumanne tarehe 10 hadi 13 Aprili, 2012 kamati mbalimbali za klabu ya michezo ya Biafra zitakuwa zikikutana kwa ajili ya kujadili na kujipanga juu ya utekelezaji wa majukumu mbalimbali yanayozigusa kamati hizo. Kwa mujibu wa katibu mkuu wa klabu hiyo ndugu Yahya Poli (Kaka Poli) kamati ya kwanza kabisa kukutana ilikuwa ni kamati ya Uchumi na Mipango ambayo ilikutana Jumanne tarehe 10 Aprili, 2012 Baadhi ya wajumbe wa Kamati hiyo ni ndugu Ibrahim Kilasa, Robert Mwakibugi, Mariam Sabaje na Maneno Juma pamoja na masuala mengine walijadili juu ya fursa mbalimbali zilizopo ambazo zinaweza kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa klabu, wanachama wake na jamii kwa ujumla. Pia kamati hiyo iliazimia kuandaa mpango mkakati wa utekelezaji wa majukumu yao.
Ibrahim Kilasa - Mjumbe wa kamati ya Uchumi na Mipango

Kamati ya Nidhamu na Rufaa ilikutana tarehe 11 Aprili, 2012 ambapo wajumbe wa kamati hiyo baadhi yao ni Mustapha Muro, Ismail Hamad, Mwajuma Usale, Adam Mwambapa na Emmy Jack ambapo kamati hiyo pamoja na masuala mengine ilianza kuainisha masuala mbalimbali ya kinidhamu na kubainisha baadhi ya vipengele vya kanuni za adhabu.  Kamati hiyo pia inaanda mpango kazi wake.

Emmy Msechu (mwenye kilemba) - Mjumbe wa Kamati ya Nidhamu na Rufaa 

Alhamisi, Aprili 12, 2012 Kamati ya Ufundi inakutana ambapo kamati hiyo, pamoja na masuala mengine itajadili na kutengeneza mpango wake. Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo ni Michael Silili, Ramadhani Said, Ally Juma, Nancy Raphael na Acholo Luvanda.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ufundi - Ally Juma (mwenye tracksuit nyekundu), Ramadhani Said (wa nne kutoka kushoto) na Michael Silili (mwenye tracksuit nyeusi)

Kamati ya Utendaji inatarajia kukutana tarehe 13 Aprili, 2012. Katika kikao hicho wenyeviti wa kamati zote tatu watashiriki na kuwasilisha kwa muhtasari waliyoyajadili na kuazimia kwenye vikao vyao. Maazimio hayo yatajumuishwa katika mpango kazi wa kamati ya utendaji na baadaye kuwasilishwa kwa wanachama wote.

Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Utendaji kutoka kulia - Jacqueline Barozi (Makamu Mwenyekiti), Henry Maseko, Abdul Mollel (Mwenyekiti) na Yahya Poli (Katibu Mkuu)

1 comment:

  1. Mungu aisaidie biafra sport club iwe club bora

    ReplyDelete