Wednesday, April 04, 2012

ICHAGUE BLOGU YA BIAFRA KATIKA TUZO ZA BLOGU ZA TANZANIA - 2012


Blogu ya klabu ya michezo ya Biafra ambayo tangu iwe hewani kwa mara ya kwanza kwa kubisha hodi mnamo mwezi Agosti, 2011 imekuwa hai na kuweka habari mbalimbali za kimichezo na afya zinazoihusu klabu ya Biafra pamoja na klabu nyingine . Mpaka tunapoandika hapa leo, blogu imeshatembelewa zaidi ya mara 1900 na watu kutoka nchi mbalimbali duniani na wengi zaidi wanazidi kuitembelea kila siku.

Baadhi ya wanabiafra wakiwa katika mazoezi ya mbio za pole pole (jogging)


Hivyo basi, klabu inapenda kuchukua fursa hii kukuomba wewe mwanachama, shabiki, mpenzi na mdau wa blogu pamoja na michezo kwa ujumla kuipigia kura blogu yetu katika 'kategori' 3 ambazo ni Blogu ya Mwaka, Blogu Mpya na Blogu ya Michezo katika Tuzo za Blogu za mwaka 2012 kwa kujaza Fomu ya Kuichagua Blogu.

Makamu Mwenyekiti wa Biafra Jaqueline Barozi (wa kwanza kushoto) na Mweka Hazina (mwenye fulana nyekundu) wakijadiliana na wanachama.

KURA YAKO NI MUHIMU SANA!!!!

No comments:

Post a Comment