Thursday, April 05, 2012

BIAFRA KIDS YAJIDHATITI KUSHIRIKI KOMBE LA COPA COCA COLA 2012 WILAYA YA KINONDONI

Klabu ya michezo ya Biafra imeiingiza timu yake ya watoto inayojulikana kama Biafra Kids a.k.a. The Juniors katika kinyan'ganyiro cha kuwania kombe la Copa Cocacola -2012 ambalo linatarajiwa kuanza juma lijalo. Akiongea kwa kujiamini nahodha wa Timu hiyo Tajuddin Hussein alisema kuwa wamejiandaa kushiriki kikamilifu na kuchukua kombe la Copa Cocacola wilaya ya Kinondoni kwani wameshiriki katika ligi mbalimbali na kuchukua vikombe na sasa ni wakati muafaka kwa timu yao kushiriki michauano mikubwa kama ya Copa Cocacola.



KIKOSI CHA BIAFRA KIDS KILIPOCHEZA NA KOMBAINI YA TIMU YA WATOTO WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU AGOSTI, 2011

 Pia wachezaji wa timu hiyo wamewaomba mashabiki wa timu yao na mchezo wa mpira wa miguu kwa ujumla kuwaunga mkono na kuwasaidia kwa hali na mali katika kufanikisha ushiriki wa timu hiyo kwenye michuano ya Copa Cocacola wilaya Kinondoni.

KIKOSI CHA BIAFRA KIDS KILIPOCHEZA NA TIMU YA WATOTO YA SIMBA
FOMU YA USAJILI WA TIMU YA BIAFRA KIDS  ILIYOWASILISHWA TFF

No comments:

Post a Comment