Monday, February 13, 2012

TAREHE YA MWISHO YA KUCHUKUA FOMU ZA UANACHAMA WA KLABU YA MICHEZO YA BIAFRA YATANGAZWA

Mwenyekiti wa klabu ya michezo ya Biafra Bw. Abdul Mollel ametangaza kwamba tarehe 15 februari, 2012 kuwa ndio tarehe ya mwisho ya kuchukua fomu za uanachama wa klabu. Tangazo hilo alilitoa mara baada ya kumaliza mazoezi ya mbio za pole pole zilizoandaliwa na kuratibiwa na klabu ya Biafra na namanga. Aliwakumbusha wanachama na wadau wengine wote kuwa tarehe hiyo imepangwa kwa kuzingatia pia kwamba klabu kwa sasa inajiandaa na uchaguzi mkuu wa kwanza wa viongozi ambao umepangwa kufanyika tarehe 11 machi, 2012.
Mwenyekiti wa Biafra Abdul A. Mollel akiongoza mazoezi ya mbio za pole pole (jogging)

No comments:

Post a Comment