Wednesday, February 08, 2012

NEMBO RASMI YA KLABU YA MICHEZO YA BIAFRA YAANZA KUTUMIKA

Katika kuirasimisha klabu yao, viongozi na wanachama wa klabu ya michezo ya Biafra wameanza rasmi kuitumia nembo mahususi ya klabu kama inavyoonekana hapo juu. Kwa kuwa klabu ina lengo la kuhamasisha michezo hususan mchezo wa mbio za pole pole ambazo hujulikana kama 'jogging' katika nembo ya klabu wanaonekana wa watu wawili wakikimbia kwa mtindo wa mbio za pole pole. Lakini bila kusahau michezo mingine, kuna picha ya mpira pamoja na ya mwanamasumbwi. Hiyo ni kwa uchache tu.

No comments:

Post a Comment