Wednesday, February 01, 2012

KLABU YA MICHEZO YA BIAFRA YAJIANDAA KUFANYA UCHAGUZI MKUU WA KWANZA WA VIONGOZI WA KLABU


RATIBA YA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA KWANZA WA VIONGOZI WA KLABU YA MICHEZO YA BIAFRA UTAKAOFANYIKA TAREHE 11 MACHI, 2012.
Mara baada ya kupata usajili rasmi toka serikalini klabu ya michezo ya Biafra imejipanga kufanya uchaguzi mkuu wa kwanza wa viongozi ambao unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 11 Machi, 2011. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa klabu hiyo Bw. Abdul Mollel, ratiba hiyo ya uchaguzi inafuatiwa na uchukuaji wa fomu za uanachama kwa mujibu wa ratiba inayoonekana hapa chini: -
Ratiba ya uchukuaji na urudishaji fomu mbalimbali
1.      Fomu za maombi ya uanachama zimeanza kuuzwa tarehe 28 Januari, 2012
2.      Tarehe ya mwisho ya kurudisha fomu za uanachama ni 15 Februari, 2012
3.      Fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi zitaanza kutolewa tarehe 19 - 22 Februari, 2012
4.      Mwisho wa kurejesha fomu za kugombea nafasi za uongozi ni tarehe 25 Februari, 2012
5.      Uchaguzi mkuu wa viongozi utafanyika tarehe 11 Machi, 2012
Nafasi za uongozi zitakazogombewa katika uchaguzi huo ni kama ifuatavyo: -
1.      Mwenyekiti
2.      Makamu mwenyekiti
3.      Katibu Mkuu
4.      Katibu Mkuu Msaidizi
5.      Mweka Hazina
6.      Wajumbe watano (5) watakaoingia kwenye kamati ya utendaji
7.      Wajumbe nane (8) wa kamati ya uchumi na mipango
8.      Wajumbe saba (7) wa kamati ya ufundi
9.      Wajumbe saba (7) wa kamati ya nidhamu na rufaa
Kwa maelezo, maoni na maswali wasiliana na katibu wa klabu kwa anuani ifuatayo: -
BIAFRA SPORTS CLUB,
SIMU: +255 715 253 653
HQ: MTAA WA ISELE, 90 DEGREES PUB,  KINONDONI
DAR ES SALAAM.





    No comments:

    Post a Comment