Tuesday, February 28, 2012

BIAFRA SPORTS CLUB YATOA SHUKRANI KWA MASHABIKI WALIOTEMBELEA BLOGU YA KLABU

Blogu ya klabu ya michezo ya Biafra ilianzishwa mnamo mwezi Agosti, 2011 ikiwa kama ni kiunganishi mahususi cha kupashana habari miongoni mwa wanachama, mashabiki pamoja na wadau wengine ulimwenguni kote. Kuanzishwa kwake kulileta hamasa kubwa miongoni mwa klabu nyingine za michezo hasa zile zinazojihusisha zaidi na mchezo wa mbio za pole pole (jogging) ambapo kufikia januari mwaka 2012 moja ya klabu iliyohamasika na kufungua blogu yao pia. Hadi kufikia mwezi Februari 2012 blogu imeshatembelewa na watu zaidi ya 1440 kutoka mataifa mbalimbali duniani kama takwimu zinavyoonesha.


Kikosi cha Biafra Kids - The Juniors

Wanabiafra wakiwa kwenye mbio za pole pole za kila jumapili

Baadhi ya viongozi na wanachama wa Biafra Sports Club


Wanachama wa Biafra Sports Club wakiingia hospitali ya mwananyamala 'kimya kimya' kwa ajili ya kufanya usafi kuadhimisha miaka 50 ya uhuru 9/12/2011

Uongozi na wanachama unatoa shukrani kwa wale wote waliopata fursa ya kutembelea blogu na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na klabu, na pia shukrani ziwaendee wanablogu pamoja na wanamtandao kwa kushirikiana kwa ukaribu kwa aidha kuweka habari mbalimbali zinazotolewa na klabu na/au kuweka kiunganishi 'link' ya blogu ya klabu kwenye menu za blogu zao kama vile Issa Michuzi, Maggid Mjengwa, Ahmad Michuzi, Shaffih Dauda, n.k.


Mwanabiafra Michael Silili akimjulia hali na kumfariji mgonjwa aliyelazwa katika hospitali ya Mwananyamala

Wanabiafra wakitoa maji na sabuni kwa wagonjwa katika hospitali ya Mwananyamala

We! We! Mazoezi ni Afya .... Acha Kujiachia!!!

Wanabiafra wakijipatia chakula pamoja na watoto wanaoishi katika mazingira magumu

Hati ya usajili wa klabu


Tuendelee kushirikiana katika kudumisha michezo, kupashana habari na kuimarisha afya zetu.

No comments:

Post a Comment