Tuesday, June 18, 2013

WANABIAFRA WAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA JUNI 16, 2013 KWA KUTEMBELEA KITUO CHA MAMA TEREZA MBURAHATI NA KUSHIRIKIANA NA WATENDAJI WA KUTO HICHO KUFANYA USAFI, KUCHEZA NA WATOTO NA KUTOA MISAADA YA KIBINADAMU KITUONI HAPO

Katika kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika tarehe 16 juni, 201 wanamichezo toka katika klabu ya Biafra waliamua kutembelea kituo cha kulelea wasiojiweza cha "Missioneries of Charity (Mother Teresa) Children's Home" Mburahati Madoto maarufu "Kwa Mama Tereza". Lengo la kutembelea la safari hiyo lilikuwa ni kujumuika pamoja na watoto wanaolelewa kituoni hapo na kutoa misaada ya kibinadamu kama vile chakula, mavazi na vifaa vya shuleni na pia kushirikiana na watendaji wa kituo hicho katika kazi mbalimbali kama vile kufanya usafi, kufua na kuwakutanisha watoto wanaolelewa kituoni hapo na watoto wenzao ili kuwa na wakati mzuri na kufurahi pamoja kucheza. 

 
Watoto wa Biafra wakiingia kwa Mama Tereza

Wanabiafra wakiingia kwa Mama Tereza
Safari ya kuelekea Kituoni hapo Ilianza saa 1:30 asubuhi kwa basi kupitia brabara ya Kawawa kisha Kigogo njia panda ya Tabata Dampo ambapo wanamichezo waliteremka hapo na kuanza mbip za pole pole kuelekea Mburahati Madoto kilipo kituo. Mara baada ya kuwasili na wanamichezo walipokelewa na Kiongozi wa kituo Sister Saviona ambaye tulimkabidhi misaada tuliyokuja nayo.   


Mratibu wa zoezi la ukusanyaji misaada Bi. Mariam Sabaje akiipanga mara baada ya kukabidhi
Zoezi la kutupa taarifa mbalimbali za kituo hicho lilifanyika na hatimaye tulipata fursa ya kuwasabahi watoto wanaolelewa kituoni hapo pamoja na watu wengine wakiwemo wazee na wafanyakazi.
Katibu Mkuu wa Biafra Yahya Poli akimsikiliza kwa makini Sister Saviona

Wanabiafra wakisikiliza historia ya Kituo cha Mama Tereza toka kwa Sister Saviona (hayupo pichani)

Katibu wa Kamati ya Ufundi Ally Juma akiongoza msafara kutembelea maeneo mbalimbali kituoni hapo

Baadhi ya watoto wanaolelewa kituoni wakichangamana na Wanabiafra

Hamza Kimathy akiwa na mtoto

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Biafra - Ally Selemani pamoja na watoto

Ally Juma




Watoto wakifurahi picha

Mhamasishaji na mwimbishaji wa Biafra Chriss Matembo (wa pili kushoto waliosimama) akiwa na Makamu Mwenyekiti na watoto

Mara baada ya kutembezwa maeneo mbalimbali na kuwasalimia watoto kazi mbalimbali zilianza kufanyika ikiwemo kufua, kufagia na kupiga deki, kufuta vumbi madirisha na pia kupiga hadithi na watoto, fuatilia matukio yote kwenye picha. 
Kutoka kushoto; Mwajuma Mohamed, Zawadi Rajab, Emmy msechu na Mariam Sabaje

Abdallah Omari (kulia) na Ibrahim Kilasa

Chriss Matembo

Vijana wakifua


Magreth Warisanga (mwenye kofia) akifua pamoja na Jaqueline Barozi

Nancy Raphael (kushoto) akisaidiana kufua

Salma Mathias aifuta dirisha


Zawadi Rajab (mwenye kitambaa) na Mariam Sabaje wakipiga deki

Salma Mathias akisuuza nguo


Henry Maseko

Makamu M/Kiti Jqueline Barozi akianika nguo

Rehema Shaban na Miriam Joseph wakinika nguo

Watoto wakicheza pamoja

Mossi Said akiwahidithia hadithi kwa watoto
Zoezi la kufanya usafi lilikamilika na wakati wa mapumziko wanabiafra waliutumia vyema kujadiliana mambo mbalimbali waliyojifunza kituoni hapo pamoja na kuzungumza na wazee wanaoishi kituoni. 



Hatimaye siku maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika kwa mwaka 2013 kwa wanabiafra yalikamilika majira ya saa 6:30 mchana kwa kuwashukuru wahusika wote katika Kituo cha Mama Tereza kutukubalia ombi letu la kuwatembelea na pia uongozi pamoja na wafanyakazi na watoto kituoni hapo walitoa shukrani kwa kuwa pamoja nao na kuomba tuwe na utaratibu wa kwenda mara kwa mara. Baada ya shukrani, safari ya kurudi klabuni ikaanza  kwa mwendo mdogomdogo hadi njia panda ya Madoto na kisha kupanda gari. 



Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya Klabu ya Michezo ya Biafra, napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wanachama wote kwa kujitolea vitu mbalimbali na kujitokeza kwa wingi. Vile shukrani za dhati ziwaendee wadau wetu Janice Mlunde na Faraja Emmanuel kwa kujitolea nguo kadhaa za watoto pamoja na sukari.
 

No comments:

Post a Comment