Sunday, June 23, 2013

HABARI NA MATUKIO YA MAZOEZI YA PAMOJA KATI YA KUNDUCHI KWANZA NA BIAFRA LEO TAR 23 JUNI, 2013

Leo tarehe 23 Juni, 2013 wanamichezo toka klabu za Kunduchi Kwanza na Biafra walifanya mazoezi ya pamoja ya mbio za pole pole ambazo zilianzia katika viwanja vya Machava Kunduchi Mtongani na kuishia makao makuu ya klabu ya Kunduchi Kwanza yaliyopo Malanja Executive Inn Kuduchi Mtongani. Lengo la kufanya kufanya mazoezi ya pamoja lilikuwa ni kudumisha uhsuiano mwema uliopo baina ya klabu hizo mbili na pia kuwasilisha mchango wa Shilingi laki moja (100,000/=) ambazo wanabiafra waliahidi kama sehemu ya kuchangia gharama za ujenzi wa Makao Makuu ya klabu ya Kunduchi baada ya kupata ajali ya kuungua moto na kuteketeza ukumbi wa mikutano na sherehe. Fuatilia matukio katika picha.







Mara baada ya kureje klabuni, wanamichezo walifanya mazoezi ya kunyoosha viungo



Mara baada ya kunyoosha mwili wanamichezo wote walijumuika pamoja kwa ajili ya zoezi la kukabidhi mchango wa Biafra kwa Kunduchi Kwanza.

Mwenyekiti wa Biafra Akizungumza

Katibu Mkuu wa Biafra akizungumza

Katibu Mkuu wa Kunduhci Kwanza Alphonsina Joseph Mbusilo (aliyesimama) akiwashukuru wanabiafra

Mwenyekiti wa Biafra akimkabidhi mchango mweka hazina wa Kunduchi Kwanza


No comments:

Post a Comment