Wednesday, June 26, 2013

BARAFU JOGGING WAFANYA JOGGING PAMOJA NA WABUNGE MJINI DODOMA

Katika harakati za kuhamasisha mchezo wa mbio za pole pole (jogging) miongoni wa watunga sheria, klabu ya  Barafu Jogging ya Magomeni Dar es Salaam ilisafiri mpaka mkoani Dodoma na kufanya jogging pamoja na wabunge wa bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Miongoni mwa wabunge walioshiriki ni pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba,  Mbunge wa Kinondoni Idd Azan, Mbunge wa Nzega Dk. Khamis Kigwangala,  Mbunge wa Namtumbo, Vita Kawawa, n.k. Angalia picha za tukio hilo. Picha zote kwa hisani ya Shaffih Dauda Blog na Barafu Jogging
Mheshimiwa Iddi Azzan akiwaelekeza waheshimiwa wenzake namna ya kupanga mistari kwa ajili ya kukimbia jogging
Kutoka kushoto mbele kabisa ni waheshimiwa Iddi Azza, Amos Makala na Hawa Ghasia

Waheshimiwa wakikatiza mitaa ya Dodoma

Mara baada ya kukamilisha mbio za pole pole na kama ilivyo ada kwa wana-jogging washiriki wote walijumuika pamoja kwa ajili ya kufanya "aerobics" ambapo washiriki hufanya mazoezi kwa kumfuata kiongozi na midundo ya muziki.
Mheshimiwa Iddi Azzan akiwaongoza waheshimwa wenzake kujipanga kwa ajili ya "aerobics"

Waheshimiwa wabunge pamoja na wa Barafu Jogging wakifanya "aerobics" picha za chini pia wakiendelea na aerobics






 
Tunawapongeza sana wenzetu wa Barafu Jogging kwa kuhamasaisha mchezo wetu pendwa wa mbio za pole pole.

No comments:

Post a Comment