Wednesday, February 20, 2013

BIAFRA SPORTS CLUB YAPATA USAJILI RASMI

Leo tarehe 20 Februari, 2013 klabu ya michezo ya Biafra imepata usajili rasmi toka Baraza la Michezo Tanzania (BMT). Usajili huo umetokana na kutimiza masharti na kanuni zote ziliyowekwa na baraza hilo katika usajili wa vilabu vya michezo nchini Tanzania. 
Cheti cha Usajili wa Biafra Sports Club
Akizungumza wakati akikabidhi cheti hicho kwa Katibu Mkuu wa Biafra ndugu Yahya Poli, Msajili wa Vyama na Vilabu vya Michezo Tanzania Mama Rwezaula aliwapongeza wanachama wote kwa kuanzisha klabu hiyo na pia aliwasihi viongozi na wanachama kuhakikisha wanasimamia na kuilinda katiba ya klabu hiyo na kujiepusha na migogoro ili kuendeleza michezo nchini.
Barua ya Usajili wa Biafra Sports Club

 Mwenyekiti wa klabu hiyo ndugu Abdul Mollel akizungumza tokea safarini Songea, aliwapongeza wanachama wote kwa kujitolea kwao katika kuiendeleza klabu na uvumilivu pale palipotokea na vikwazo vya hapa na pale. 

HONGERA WANABIAFRA WOTE - SASA TUJENGE KLABU YETU KWA KUINUA NA KUHAMASISHA MICHEZO, UPENDO, UMOJA NA USHIRIKIANO!!!!

No comments:

Post a Comment