Monday, February 11, 2013

MATUKIO YA WANABIAFRA KATIKA WIKINDI ILIYOPITA

Wanamichezo takriban wote wana msemo wao kuwa "michezo ni afya, michezo ni furaha, michezo huwaunganisha watu". Basi hivyo ndivyo ilivyokuwa juma lililopita kwa Wanabiafra. Siku ya ijumaa tarehe 8 Februari, 2013 ambapo Wanabiafra pamoja na marafiki kadhaa walikutana na kuianza wikiendi kwa burudani ya muziki, vinywaji na nyama choma pale Chiminga Unique Pub. 
Ally Masharubu na Ayub Layson wakitafuna nyama ya mbuzi

Mwenyekiti wa Biafra Abdul Mollel alisimama kuwasalimia wanabiafra na marafiki

Kutoka kushoto; Ally Masharubu, Ayub Layson na Editha Tungaraza

Mwanabiafra Dustan Barozi (kulia) pamoja na marafiki zake

Editha Tungaraza akifaidi msosi

Makamu Mwenyekiti wa Biafra Jacqueline Barozi (aliyesimama) akichukua oda ya vinywaji


Rose Mwakibugi Almaarufu mama Chimbinga alihakikisha vinywaji vipo na vya kutosha

Robert Mwakibugi akiiwakilisha vyema Chimbinga Unique Pub
Kama unapenda kushiriki kwenye mijumuiko ya aina hii, usisite, wasiliana na Katibu Mkuu, Biafra Sports Club kwa barua pepe; biafra.jsclub@gmail.com

No comments:

Post a Comment