Thursday, February 28, 2013

JOGGING YAVIKUTANISHA TENA VILABU KUNDUCHI JUMAPILI TAREHE 3 MACHI, 2013

Katika kuhamasisha mchezo wa mbio za pole pole (jogging) maeneo ya Kunduchi na kuimarisha uhusuiano wa vilabu vya jogging, Jumapili ya tarehe 3 Machi, 2013 wanamichezo kutoka katika vilabu vya Namanga, Kawe, Biafra na Kunduchi Kwanza pamoja na wadau wengine wa michezo watajumuika na kufanya mazoezi ya pamoja ya jogging ambayo yataratibiwa na klabu ya Kunduchi Kwanza ambao ndio wenyeji na waratibu wa mazoezi hayo. 
Jogging
 

Jogging ikiendelea

Baada ya mazoezi hayo, wanamichezo wote waliohudhuria watajumuika pamoja makao makuu ya klabuya Kunduchi yaliyopo Malanja Pub ambapo kutafanyika na kikao cha pamoja cha viongozi vilabu shiriki juu ya mustakbali wa mchezo wa mbio za pole pole wilaya ya Kinondoni ikifuatiwa na burudani mbalimbali.

Wadau wote mnakaribishwa!


No comments:

Post a Comment