Thursday, July 05, 2012

TANZIA: MWANABIAFRA ASHA YUSUF AFIWA NA BABA YAKE MZAZI LEO TAREHE 5 JULAI, 2012

Klabu ya michezo ya Biafra, kwa masikitiko makubwa inapenda kuwatangazia wanachama, wadau, mashabiki na wapenda michezo kwa ujumla kwamba mwanachama mwenzao ASHA YUSUPH (pichani chini) amefiwa na BABA YAKE MZAZI asubuhi ya leo tarehe 5 Julai, 2012 katika hospitali ya Mwananyamala.
ASHA YUSUPH (WA KWANZA KUSHOTO) AKIWA NA EDITHA TUNGARAZA NA NANCY RUPIA

Akizungumza na Katibu wa Biafra, Asha aliwaarifu wadau wote kwamba, msiba utakuwa nyumbani kwa marehemu Kinondoni Shamba na mazishi yatafanyika kesho jioni huko shambani kwa marehemu Kongowe (mbagala) Dar es Salaam.
Asha Yusuf (wa tano toka kushoto waliosimama mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na Wanabiafra

Kwa niaba ya wanachama na wadau wote wa Biafra, mwenyekiti anatoa pole kwa mwanachama mwenzetu pamoja na ndugu, jamaa na rafiki zake kwa msiba huo na pia kuwaomba Wanabiafra wote kumfariji mwanachama mwenzao. Kwa mawasiliano, namba ya Asha Yusuph ni 0659327117.

Inna Lillahi - Wa Inna Ilaihi Raaji'un, Bwana Ametoa, Bwana Ametwaa; Jina lake Lihimidiwe.

No comments:

Post a Comment