Tuesday, July 17, 2012

KATIBU WA KAMATI YA UFUNDI YA BIAFRA AFUNGA NDOA!!!

Siku jumamosi tarehe 14 Julai, 2012 ilikuwa ni siku ya furaha sana kwa mwanabiafra Ally Juma ambaye ni katibu wa Kamati ya Ufundi ya klabu hiyo baada ya kufunga ndoa na Bi Zahra Iddi. Ndoa hiyo ilifungwa nyumbani kwa familia ya bi harusi Tegeta Msikitini na sherehe iliyofana kufanyika katika ukumbi wa 90 Degrees Pub ambako ni makao makuu ya klabu ya michezo ya Biafra.

Bwana na Bi harusi baada ya kuingia ukumbini wakiwa pamoja na wapambe wao

Baadhi ya wanabiafra wakiongozwa na makamu mwenyekiti Jackline Barozi (mwenye gauni jeusi)

Katibu wa Biafra Kaka Poli akiwakaribisha wageni ukumbini pembeni ni MC wa sherehe hiyo

Bwana harusi ambaye ni katibu wa kamati ya ufundi ya klabu akimtambulisha Mwenyekiti wa Kamati hiyo ndugu Michael Silili 

Maharusi wakilishana keki 


Mwenyekiti wa Biafra Abdul A. Mollel akila keki kwa niaba ya klabu 

Wanabiafra wakijadiliana
Wanabiafra waliohudhuria sherehe hiyo wakiongozwa na Katibu Kaka Poli

Baadhi ya wageni waalikwa

Kwa niaba ya wanachama, viongozi, mashabiki na wadau wote, klabu inatoa pongezi za dhati kwa maharusi na kuwaoombea mwenyezimungu aibariki ndoa yao.



No comments:

Post a Comment