Thursday, July 12, 2012

BIAFRA DAY 2012 YASOGEZWA HADI SEPTEMBA KUPISHA ZOEZI LA SENSA YA WATU

Katibu Mkuu wa klabu ya michezo ya Biafra ndugu Yahya Poli ameutangazia umma kwamba BIAFRA DAY 2012 ambayo awali ilipangwa kufanyika tarehe 26 Agosti, 2012 sasa imesogezwa mbele hadi tarehe 2 Septemba, 2012. Kusogezwa huko mbele kwa juma moja kumetokana na siku ya awali tarehe 26 Agosti, 2012 itakuwa ni siku maalum ya Sensa ya watu na makazi nchini Tanzania.
Wanabiafra wakikatiza eneo la daraja la salender wakiwa kwenye mazoezi ya mbio za polepole


Akielezea zaidi, ndugu Poli alitanabaisha kwamba mipango ya kufanikisha BIAFRA DAY 2012 bado inaendelea na kuwakaribisha wadau wote ambao wangependa kushiriki siku hiyo kwa ufadhili na udhamini wasisite kuwasiliana na viongozi wa klabu kwa kuwa fursa bado ipo. Pia alitoa msisitizo kwa kamati zote za klabu kukutana kwa ajili ya kuendelea na maandalizi ya BIAFRA DAY, 2012. 
BIAFRA DAY 2011 - Wanabiafra wakishindana kuvuta kamba



  

No comments:

Post a Comment