Sunday, August 18, 2013

MAZOEZI YA JOGGING TARE 18 AGOSTI, 2013 YAZIKUTANISHA TENA BIAFRA NA NAMANGA

Katika kuimarisha mahusiano na ujirani mwema kwa vilabu vya jogging, wanamichezo kutoka vilabu vya Biafra na Namanga vilifanya mazoezi ya pamoja ambayo yalianzia mtaa wa Isere na kuingia barabara ya Kawawa hadi barabara ya kuelekea kwa Kopa mpaka kwenye makutano ya barabara ya Mwananyamala kuelekea Viktoria, kisha barabara ya Bagamoyo hadi Sayansi kwenye makutano ya barabara ya Rose Garden (Tembo Avenue) kutokea kwa Nyerere, kisha kufuata barabara ya Mwai Kibaki hado Moroko kuelekea Biafra na kumalizia klabuni. Fuatilia matukio kwa picha.
Tulikutana na vijana wa Mwendo Kasi Jogging (wenye jezi nyekundu)

Tulipata bahati ya kukutana na bibi ambaye alituunga mkono kwa kukimbia pamoja nasi







WOTE MNAKARIBISHWA KATIKA MAZOEZI YA MBIO ZA POLE POLE! 

MAZOEZI NI AFYA, ACHA KUJIACHIA!!!


No comments:

Post a Comment