Monday, August 12, 2013

HAFLA YA IFTAR YA WANABIAFRA KATIKA MATUKIO

Tarehe 8 Agosti, 2013 ambayo pia ilikuwa 30 Ramadhan, 1434 klabu ya michezo ya Biafra iliandaa hafla ya kushiriki pamoja katika iftar na kuuaga mwezi mtukufu wa Ramadhan. Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Mheshimiwa diwani wa kata ya Mwananyamala ndugu Songoro Mnyonge pamoja na wageni waalikwa toka vilabu mbalimbali vinavyojihusisha mchezo wa mbio za pole pole (jogging), waandishi na watangazaji wa habari za michezo, wanablogu na wadau mbalimbali wa klabu ya Biafra.
Waheshimiwa Songoro Mnyonge (diwani wa mwananyamala) kulia na Faustine Makima M/Kiti serikali ya mtaa wa Balozi Msolomi/Isere

Mwenyekiti wa Kunduchi Kwanza Jogging Asia Mohamed (kulia)

Wanachama wa Kawe Social and Sports Club wakiwakilisha

Wawakilishi toka Kopa Generation Jogging

Watoto wa Biafra

Iftar ikiendelea






Watoto wa Biafra wakipata iftar

Wadau na mashabiki wa Biafra wakipata Iftar

Mhamasishaji na mwimbishaji wa Biafra Chriss akipata iftar

Katibu wa Biafra Kaka Poli akipata iftar


Mhamasishaji wa Biafra Kaka Hamza akipata Iftar

Katibu wa Kamati ya Ufundi ya Biafra Ally Juma akipata Iftar
Mheshimiwa Songoro Mnyonge - Diwani wa Mwananyamala akitoa neno la shukrani
Baada ya kumaliza hafla ya Iftar, mgeni rasmi katika hafla hiyo Mheshimiwa Diwani, Songoro Mnyonge  alipata wasaa wa kutoa neno la shukrani kwa Wanabiafra na pia kwa washiriki wote katika hafla hiyo ambapo pamoja na mambo mengine alieleza kufuruhaishwa sana tukio hilo na hivyo kumpa hamasa yeye ya kuona namna anavyoweza kushirikiana na klabu katika kuhamasisha michezo na maendeleo miongoni mwa wanajamii. Pia alitumia fursa hiyo kuelezea kinagaubaga nia yake ya kuwa mwanachama wa klabu ya michezo ya Biafra. Wanabiafra walipokea maombi ya mheshimiwa Diwani kwa shangwe na faraja na kumkaribisha rasmi katika klabu yao.
Katibu wa Biafra akiagana na wageni mheshimiwa Diwani (katikati) na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa
Klabu ya michezo ya Biafra inatoa shukrani za dhati kwa wadau wote waliofanikiwa kushiriki moja kwa moja katika hafla ya Iftar wakiwemo marafiki kutoka vilabu mbalimbali. Tumefurahi kujumuika pamoja, karibuni sana!

No comments:

Post a Comment