Thursday, August 01, 2013

BELLE 9, YOUNG KILLER, BRIGHT NA WASANII KIBAO KUTUMBUIZA KATIKA MIJI YA MBEYA NA TUNDUMA SIKUU YA IDD MOSI NA IDD PILI

Katika kuwasogezea burudani karibu kabisa, kampuni ya Robik General Supplies Ltd imeandaa maonyesho ya muziki kwa wakazi wa miji ya Mbeya, Tunduma na maeneo ya jirani katika kusherehekea sikuu ya Idd mosi na Idd pili. Akizungumza na mwandishi wetu, mkurugenzi wa Robik ndugu Robert Mwakibugi alieleza kwamba sikukuu ya Idd mosi na Idd pili burudani itatolewa na wasanii Belle 9 Young Killer, Bright na wengineo ambapo Idd mosi onyesho litafanyika katika ukumbi wa Honeymoon Hotel mjini Tunduma na Idd pili onesho litafanyika katika ukumbi wa Mtenda Sunset Hotel Mbeya mjini. 

Mratibu wa matukio wa kampuni hiyo ndugu Boniface Harrison amebainisha kwamba kila kitu kinakwenda vizuri na tayari wasanii wote wamethibitisha kushiriki katika maonesho hayo ambayo yanadhaminiwa na Mtenda Sunset Hotel & Conference Centre, Honeymoon Hotel pamoja na Chimbinga Unique Pub. Pia alitoa fursa kwa wadhamini wengine kujitokeza kudhamini maonesho hayo.  

No comments:

Post a Comment