Monday, October 15, 2012

BIRTHDAY YA KAWE JOGGING YAFANA

Klabu ya mchezo wa mbio za pole pole ya Kawe jana tarehe 14 Oktoba, 2012 ilitimiza mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake ambapo mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Mh. Anjela Kairuki (Mb.). 
WanaKawe Jogging

Wanamichezo kutoka vilabu mbalimbali walishiriki katika hafla hiyo ambayo ilianza kwa mazoezi ya mbio za pole pole yaliyoanzia na kuishia katika vwanja vya Tanganyika Packers na hatimaye michezo mingine ya kuvuta kamba, kukimbiza kuku na soka la vijana ambapo Biafra Youth Football Team ilitoka sare ya bila kufungana na timu ya vijana ya Kawe.

Mara baada ya michezo kumalizika wanamichezo wote walijumuika pamoja katika ukumbi wa Massae Pub ambapo ndipo yalipo makao makuu ya Kawe jogging kwa shguli nyinginezo zilizoenda sambamba na hafla hiyo.
 


No comments:

Post a Comment