Thursday, October 11, 2012

BIAFRA JOGGING YAALIKWA KUSHIRIKI SHEREHE KUTIMIZA MWAKA MMOJA TANGU KUANZISHWA KWA KAWE JOGGING



Katika kuadhimisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwa klabu ya Kawe Jogging, wanachama wa klabu hiyo wamealika klabu mbalimbali zinazojihusisha na uhamasisjaji wa mchezo wa mbio za pole pole mkoa wa Dar es Salaam katika kusherehekea maadhimisho hayo. Biafra Jogging, Mzimuni Jogging, Kunduchi Kwanza Jogging na klabu ni nyinginezo kwa pamoja zitafanya mazoezi ya mbio za pole pole na kisha kushiriki katika michezo mingine kama vile kuvuta kamba na  mpira wa miguu kwa wanawake na wanaume.

Wana-Kawe Jogging wakiwa katika Magofu ya Kaole mwanzoni mwaka 2012


Biafra Jogging wakiwa pamoja na Namanga Jogging mazoezini
Klabu ya michezo ya Biafra inatoa pongezi za dhati kwa Kawe Jogging na wanachama wake wote katika sherehe hizo za kutimiza mwaka mmoja. 

WE! WE! MAZOEZI NI AFYA, ACHA KUJIACHIA

No comments:

Post a Comment