Tuesday, September 25, 2012

BIAFRA YOUTH FOOTBALL TEAM INAKUOMBA UCHANGIA VIFAA VYA MICHEZO ILI KUENDELEZA VIPAJI VYA SOKA KWA VIJANA

Timu ya vijana ya Biafra inawaomba wadau wote wa michezo uwezeshwaji wa vifaa vya michezo kwa ajili ya kuimarisha vipaji vyao na kulisaidia taifa kwa siku za usoni. Akizungumza baada ya mazoezi ya timu yao katika viwanja vya Biafra Kinondoni nahodha hiyo Hussein Tahidin (pichani chini) alisema timu yao zaidi ya kucheza mpira na kukuza vipaji vyao lakini pia wanapata fursa ya kuwa pamoja kama marafiki na kujiondoa kwenye vishawishi mbalimbali na tabia zisizofaa kwenye jamii. 
Hussein Tahiddin - Nahodha
 Wakibainisha mahitaji yao, nahodha huyo pamoja na wachezaji wenzake wameeleza kwa masikitiko kuwa wanahitaji mipira, jezi, viatu, soksi, koni za mazoezi, nyavu za magoli pamoja na vifaa vingine vya michezo kwa kadri wadau watakavyoona vinafaa kwa wachezaji hao. 




Pia kwa kupitia uongozi wa klabu yao ya Biafra Sports Club vijana hao wanaomba udhamini wa timu yao ili waweze kushiriki mashindano mbalimbali ili waweze kupima uwezo wao.

MDAU! KAMA UMEGUSWA NA MAOMBI YA VIJANA HAWA NA UNGEPENDA KUWASAIDIA, UNAWEZA KUWASILIANA NA KATIBU MKUU WA BIAFRA SPORTS CLUB KWA SIMU +255 715 253 653, BARUA PEPE: biafra.jsclub@gmail.com

MISAADA YOTE ITAKAYOTOLEWA ITATANGAZWA HAPA!

1 comment: