Monday, June 18, 2012

BIAFRA KIDS YAIZAMISHA TEMEKE KIDS KWA MABAO 3 - 0

Katika kujiweka fiti kwa ajili ya kushiriki michuano ya Winome mwezi Julai mwaka 2012, timu ya Biafra Kids ilichuana na Temeke Kids katika uwanja wa Zakheem Mbagala. Mechi hiyo iliyochezwa majira ya saa sita mchana ilishuhudiwa na watazamaji zaidi ya mia tano ambao ni wanamichezo kutoka katika vilabu mbalimbali vya michezo mkoani Dar es Salaam.

Kikosi kazi cha Biafra Kids




Mchezaji wa Soka Aziza (Biafra Ladies) mwenye suruali nyeusi akifuatilia mechi kwa makini


Biafra Kids wakitoka uwanjani kwa mapumziko

Pamoja na uwanja kuwa na michanga mingi, vijana walionyesha kandanda safi kiasi cha kushangiliwa muda wote na hadi mpira unakwisha Biafra Kids walikuwa washindi wa mechi hiyo kwa mabao 3 - 0.



No comments:

Post a Comment