Monday, November 28, 2011

KATIKA KUSHEREHEKE MIAKA 50 YA UHURU - BIAFRA SPORTS CLUB YAKUSUDIA KUFANYA USAFI WA MAZINGIRA NA KUTOA MISAADA KATIKA HOSPITALI YA MWANANYAMALA TAREHE 9 DISEMBA, 2011

BAADHI YA VIONGOZI WA KLABU ZA BIAFRA, NAMANGA NA KUNDUCHI KWANZA

Klabu ya michezo ya Biafra kwa kushirikiana na klabu za michezo za Namanga na Kunduchi Kwanza wanawakaribisha wanamichezo, wadau wa michezo na wananchi kwa ujumla katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira pamoja na kutoa misaada katika hospitali ya Mwananyamala ambayo ni Hospitali ya wilaya ya Kinondoni.

Zoezi hilo la kufanya usafi na kutoa misaada katika hospitali hiyo ni katika kutimiza wajibu wetu kama jamii hasa katika kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzani ambao kilele chake kitakuwa tarehe 9 Disemba, 2011. Kamati teule ya maandalizi ya shughuli hiyo inakaribisha maoni, mapendekezo, ushauri, michango na misaada kutoka kwa watu wote watakaoguswa na dhamira hii kwa kuwasiliana na Katibu wa Biafra Sports Club ndugu Yahya Poli: +255 715 253 653, au tuandikie barua pepe biafra.jsclub@gmail.com

Kauli mbiu ya sherehe za miaka 50 ya uhuru kwa mwaka huu 2011 ni TUMETHUBUTU, TUMEWEZA, TUNASONGA MBELE! MICHEZO NI AFYA, MICHEZO USHIRIKIANO, MICHEZO NI UMOJA! 

No comments:

Post a Comment